• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

Wananchi Dar Kunufaika na Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia

Posted on: June 14th, 2025

Wananchi Mkoani Dar es Salaam wanatarajiwa kupata manufaa makubwa kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia inayotarajiwa kuzinduliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa Juni 16, 2025 katika viwanja vya Maturubai Mbagala jijini hapo.

Hayo yamebainishwa leo Juni 14, 2025 na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Miundombinu Mhandisi Amani Mafuru ambaye amemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa watoa huduma za Msaada wa Kisheria katika Kampeni hiyo.

Mhandisi Mafuru amesema, “kupitia Kampeni hii Dar es Salaam tutanufaika sana kwani migogoro na changamoto za kisheria zinazowakabili wananchi wetu zita tatuliwa bure na hivyo kuwafanya wananchi wapate muda wa kutekeleza majukumu yao mengine ya maendeleo hivyo basi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam itatoa ushirikiano wa kutosha katika utekelezaji wa kampeni hiyo”.

Ameongeza kuwa watoa huduma hao ambao wanapata mafunzo wanapaswa kuzingatia wajibu wao na kutekeleza majukumu yao kikamilifu ili nia ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan ya kuwasaidia wananchi katika sekta ya sheria itimie huku akiongeza kuwa elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kisheria bado ni changamoto kubwa kwa wananchi.

Naye Mkurugenzi wa Huduma za Msaada wa Kisheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Bi Ester Msambazi ameeleza kuwa kupitia mafunzo hayo, watoa huduma za msaada wa kisheria wataweza kubainisha maeneo ya kutilia mkazo wakati wa utekelezaji wa kampeni pamoja na kuainisha mbinu za kuwafikia wananchi wengi wenye uhitaji wa msaada wa kisheria.

Msambazi amesema kutakuwa na ukusanyaji wa takwimu mbalimbali za migogoro na huduma zitakazotolewa ambapo takwimu hizo zitasaidia katika uandaaji wa taarifa kuhusu utekelezaji wa kampeni na kuonyesha maeneo ambayo mkoa wa Dar es Salaam watayachukua kwa ajili ya maboresho na yale ya kitaifa Wizara itayabeba.


Mafunzo ya watoa huduma katika kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia yamejumuisha mawakili wa kujitegemea, mawakili wa serikali, wasaidizi wa kisheria, maafisa ardhi, maafisa ustawi wa jamii, maafisa kutoka Polisi Dawati la Jinsia, wasajili wasaidizi na wasaidizi wa Kamishna wa ardhi.


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Ukatili Kinara Migogoro inayohitaji Msaada wa Kisheria-Waziri Mkuu

    June 16, 2025
  • Wananchi Dar Kunufaika na Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia

    June 14, 2025
  • RC Chalamila, Samia Legal Aid Kuzinduliwa Juni 16, 2025 DSM

    June 13, 2025
  • Wataalam Kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Wakutana na Kamati ya Usalama ya Mkoa-DSM

    June 11, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa