• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Biashara
    • Utalii
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

Historia

HISTORIA YA JIJI LA DAR ES SALAAM

Jiji la Dar es Salaam lilianza kama Kijiji kidogo cha wavuvi kilichojulikana kama Mzizima. Kijiji hiki kilianzishwa na Wabalawa ambao walichanganyika na Wazaramo kuelekea kwenye maeneo ya Bara la Afrika Mashariki na ambazo zilijulikana kama ‘Caravan Routes’. Ujenzi wa Makao ya Sultani pamoja na bandari ulianza rasmi mwaka 1865 katika eneo la kijiji cha Mzizima. Ujenzi huo ulikamilika mwaka 1866 na Sultani Majid bin Said kuhamia Dar es Salaam mwaka huo.

Mara baada ya Sultani Majid bin Said kuhamia Dar es Salaam mji ulianza kupanuka na uchumi wake kukua kwa kasi kubwa japo kwa kipindi kifupi ambapo Sultani Majid bin Said alifariki mwaka 1870. Kifo cha Sultani huyo kilisababisha kudidimia kwa maendeleo ya mji wa Dar es Salaam. Hali hiyo ilianza tena kubadilika mwaka 1884 kufuatia kuanzishwa kwa koloni la Wajerumani la Afrika Mashariki. Mwaka 1891

Serikali ya kikoloni ya Kijerumani iliamua kuhamisha makao makuu ya utawala wake katika Afrika Mashariki kutoka Bagamoyo na kuyaweka Dar es Salaam. Hata hivyo, baada ya Wajerumani kushindwa na Waingereza katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia mwaka 1916, Mji wa Dar es Salaam uliendelea kuwa makao makuu ya utawala wa koloni la Waingereza nchini Tanganyika hadi ilipojipatia uhuru wake mwaka 1961. Dar es Salaam iliendelea kuwa makao makuu ya Tanganyika huru na hatimaye kuwa makao makuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hadi mwaka 1972 wakati Serikali ilipoamua kuhamishia makao yake makuu mjini Dodoma. Jiji la Dar es Salaam liliendelea kubaki kuwa maarufu kwa kuwa Jiji kuu na kitovu cha biashara nchini Tanzania.

Hadhi ya Mji, Manispaa na Jiji

Mji wa Dar es Salaam ulitangazwa kuwa Mji wenye Serikali yake ya Mitaa mwaka 1920. Hadhi ya Mji wa Dar es Salaam ilipandishwa kuwa ya Manispaa mwaka 1949 nabaadaye kutunukiwa hadhi ya Jiji na Malkia wa Himaya ya Uingereza tarehe 10 Desemba 1961 mara baada ya Tanganyika kupata uhuru wake. Kuanzia kipindi hicho, Jiji la Dar es Salaam lilikuwa likiongozwa na Halmashauri ya Jiji hadi mwaka 1972 wakati ambapo Serikali ilivunja Serikali zote za Mitaa nchini ili kutekeleza mfumo wa madaraka Mikoni. Mamlaka za Miji zilirejeshewa madaraka mwaka 1978 ambapo Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam lilianza kufanya kazi tena.

Serikali za Mitaa

Kabla ya Ukoloni walitawala Machifu na Wazee wa mila. Wakati wa Utawala wa Wajerumani (1884-1917) utawala wa kikoloni ulikuwa wa moja kwa moja zaidi maeneo ya mijini “Direct rule”. Katika kipindi cha utawala wa Waingereza (1917-1961) katika mwaka 1926 kulikuwa na utawala wa kikabila. Sheria ya Serikali za Mitaa zilianza mwaka 1953 na Sheria ya Miji mwaka 1946. Baada ya mwaka 1961 uliondolewa Utawala wa Machifu na kuanza Mfumo wa pamoja wa Serikali za Mitaa. Mwaka 1972 Serikali za Mitaa ziliondolewa na kuanza Utawala Mijini na mwaka 1982 Sheria ya Serikali za Mitaa zilirejeshwa tena. Mwaka 1984 ulirejeshwa mfumo wa Serikali za Mitaa na kudumu hadi mwaka 1995. Mpango wa uboreshaji wa Serikali za Mitaa kuzifanya ziwe na uwezo wa utendaji, uwazi na uwajibikaji ulianzishwa mwaka 1996 uliojulikana kama “Local Government Reform Programme”.

Mkoa wa Dar es Salaam wenye eneo na km za mraba 1,800 ulianzishwa kutoka Mkoa wa Pwani mwaka 1973 ukiwa na Wilaya 3 za Ilala, Kinondoni na Temeke. Mamlaka za Serikali za Mitaa za Mkoa wa Dar es Salaam zilizopo sasa zilianzishwa mwaka 2000 baada ya kuvunjwa kwa Tume ya Jiji iliyokuwepo kufuatia kuvunjwa kwa Serikali za Mitaa mwaka 1996 kulikoendelea hadi mwishoni mwa mwaka 1999.

Matangazo

  • FOMU YA KUHUISHA MAJUKWAA YA KUWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI DSM November 09, 2022
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Ratiba ya Mtihani wa Kumaliza Kidato cha Sita (ACSEE) - 2020 June 12, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 Shule za Sekondari za Serikali December 18, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Makalla Masoko Mapya Yatakayojengwa Washirikishwe Machinga na Viongozi wa Soko

    March 11, 2023
  • RC Makalla Aeleza Kishindo Cha Rais Dkt Samia Suluhu Miaka 2 DSM

    March 10, 2023
  • RC Makalla Atimiza ahadi ya Kuwapeleka Viongozi wa Machinga Taifa Kigali Rwanda

    March 10, 2023
  • RC Makalla Hakuna Fremu Soko la Kariakoo Zilizogawiwa Epukeni Matapeli

    March 26, 2023
  • Tazama zote

Video

RC Makalla akikagua Maendeleo ya Ujenzi na ukarabati wa Soko la Kariakoo
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa