• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

TEHAMA

Kitengo Cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano

Kitengo Cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kina lengo la kutoa huduma za kitaalamu juu ya matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano kwa Sekretarieti ya Mkoa, Aidha Kitengo hiki kinaongozwa na Mchambuzi wa Mifumo ya Kompyuta Mkuu ambaye anawajibika kwa Katibu Tawala wa Mkoa.

Majukumu ya Kitengo

Majukumu ya Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano:

  • Kutayarisha mpango Mkakati wa kuhusu teknolojia ya habari na mawasiliano, Miongozo na taratibu kwa kuzingatia Sera ya Taifa ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.
  • Kuishauri Menejimenti ya Sekretarieti ya Mkoa juu ya masuala yanayohusiana na sera zinazohusiana na teknolojia ya habari na mawasiliano na utekelezaji wa dhana ya serikali mtandao.
  • Kuishauri Menejimenti ya Sekretarieti ya Mkoa juu ya masuala yanayohusiana na sera, miongozo na taratibu zinazohusiana na takwimu.
  • Kusimamia maendeleo ya teknolojia ya habari na mawasiliano na utekelezaji wake kwa ajili ya Sekretarieti ya Mkoa.
  • Kushirikiana na OWM-TAMISEMI kuratibu na kuendeleza viwango vya teknolojia ya habari na mawasiliano kwa ajili ya “software na hardware” kwa matumizi ya Sekretarieti ya Mkoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.
  •  Kuziwezesha Mamlaka za Serikali za Mitaa katika kuendeleza na kutekeleza  mipango/miradi ya teknolojia ya habari na mawasiliano.
  • Kuratibu utekelezaji wa usanifu na kutunza/kuiendeleza matumizi yanayohusiana na Tovuti na utunzaji wa kumbukumbu kwa ajili ya Sekretarieti ya Mkoa.
  • Kutoa na kuratibu msaada wa teknolojia ya habari kwa Sekretarieti ya Mkoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.
  • Kutathimini, kuboresha na kusimamia teknolojia ya habari na mawasiliano na usimamizi wa mifumo ya taarifa/habari iliyosimikwa/iliyowekwa kwenye Sekretarieti ya Mkoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.
  • Kufanya tathimini ya mahitaji ya mafunzo juu ya usimamizi wa mifumo ya taarifa na teknolojia ya habari na mawasiliano na kuandaa mpango wa kujenga uwezo
  • Kufanya tathimini ya hatari/hasara zinazohusiana na miundombinu ya teknolojia ya habari na mawasiliano na mfumo wa usimamizi wa taarifa na namna ya kuthibiti.
  • Kuendeleza na kutunza Tovuti ya Mkoa.
  • Kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano kwenye kushughulikia takwimu na taarifa
  • Kuandaa taarifa, kutunza, kuzipitisha hatua mbalimbali, kuzichambua, kuziwasilisha, kuzisambaza na kuzihifadhi.
  • Kushirikiana na Tume ya Taifa ya Takwimu juu ya masuala yote yanayohusu Mfumo wa Taifa wa Takwimu.
  • Kuandaa masuala yote yanayohusiana na takwimu kwenye Sekretarieti ya Mkoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.


Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ni nyenzo muhimu, ambayo mchango wake ni mkubwa katika kuharakisha kufikiwa kwa Malengo ya Milenia ifikapo mwaka 2025. Kukua kwa teknolojia katika Mkoa wa Dar es Salaam, kuna mchango muhimu katika kuhakikisha kuwa wananchi wanapata taarifa kuhusu shughuli mbalimbali za utawala, sera na mipango kwa wakati mwafaka, hivyo kuwashirikisha wananchi moja kwa moja katika maamuzi yanayoathiri maisha yao. TEHAMA inatumika kila mahali na katika utoaji wa huduma za aina yoyote ile ikiwemo Elimu (Distant Learning, eLibrary), matibabu (telemedine), biashara (eCommerce, eBanking, nk),Ukusanyaji wa mapato, uongozi/utawala (eGovernace) n.k.
 
Kutokana na kuingia kwa utandawazi, dunia sasa imekuwa kama kijiji kimoja tena kidogo sana, kwani mawasiliano yamekuwa yakiboreshwa siku hadi siku na kuwa rahisi.

Mifumo(MIS) mbalimbali katika Mkoa:

  1. IFMIS- Epicor
  2. LGRCIS
  3. HCMIS-LAWSON
  4. SBAS
  5. PlanRep
  6. LGMD









Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa