• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

Wana- Dar es Salaam Tumuunge Mkono RC Makalla

Posted on: March 2nd, 2022

Mkuu wa Mkoa Mhe Amos Makalla akishiriki usafi wa pamoja februari 26, 2022 kariakoo Ilala Jijini Dar es Salaam.


Na, Bornwell Kapinga IO- DSM

Jiji la Dar es Salaam kwa mara ya kwanza tangu Taifa la Tanzania lipate Uhuru limetajwa kuwa Jiji la Sita kwa Usafi Afrika kufuatia taarifa ya kitafiti iliyotolewa na  “Africa Tours”, chanzo hicho kimebainisha Majiji 12 Safi katika Afrika “Top 12 cleanest Cities in Africa” ambapo  Jiji  namba 1. Kigali – Rwanda, 2. Port Louis- Mauritius, 3. Cape Town- South Africa, 4. Tunis- Tunisia, 5.Windhoek-Namibia, 6. Dar es Salaam –Tanzania, 7. Gaborone- Botswana, 8. Algiers- Algeria, 9. Nairobi- Kenya, 10. Libreville- Gabon, 11. Kumasi-Ghana, na 12. Asmara- Elitrea

Kwa upande wa Afrika Mashariki ukizingatia mtiririko uliotolewa na “Afica Tour” unakuta Jiji la Dar es Salaam ni la Pili kwa Usafi kwa hiyo wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam na Tanzania kwa  Ujumla wanapaswa kujipongeza na kuweka jitihada za kwenda mbali Zaidi ikibidi kufikia nafasi ya kwanza

Nimelazimika kuandika Makala hii nikilenga kubainisha Mkakati wa Usafi na Uhifadhi wa Mazingira Mkoa wa Dar es Salaam Uliozinduliwa na Mhe Amos Makalla ambao unachagizwa na Kauli mbiu ya SAFISHA PENDEZESHA DAR ES SALAAM kwa hakika ndio umepelekea Jiji la Dar es salaam kushika nafasi ya Sita kwa Usafi miongoni mwa majiji 12 Safi katika Afrika.

Wana Dar es Salaam wanapaswa kutambua Ukiongelea Tanzania unaongelea Jiji la Dar es Salaam kwa kuwa Dar es Salaam ndilo jiji la kibiashara, ndio lango la Nchi, Bandari kubwa, Uwekezaji mkubwa na Wageni wa nchi mbalimbali Duniani wanaotoka na kuingia, hata kama wanaenda sehemu nyingine lazima watapitia Dar es Salaam,

Kwa mantiki hiyo wakazi wa Dar es Salaam wanapaswa kumuunga mkono RC Makalla ambaye ndiye anaye mwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan katika Mkoa huu.

Mkuu wa Mkoa Mhe Amos Makalla katika kuhakikisha anaacha alama katika Mkoa wa Dar es Salaam amekuwa na mikakati na mbinu nyingi katika suala la usafi, alianza na kuwapanga vizuri wafanya biashara wadogo alimaarufu “Wamachinga” hapo awali kulikuwepo na utitiri wa biashara holela kila kona ya mkoa, ilifikikia hata barabara za watembea kwa miguu zilikuwa hazipitiki, vibanda vilijengwa ovyo kila sehemu, shughuli za kina mama lishe nazo zilikuwa zinafanyika kiholela hata kwenye taasisi za umma nako kulizingirwa na wamachinga kwa mfano IFM na CBE hali hiyo ilikuwa chanzo kikubwa cha uchafu katika Jiji la Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa pasipo kutumia nguvu aliwataka wafanyabiashara hao kwenda katika maeneo rasmi yaliyotengwa kwa ajili yao katika kila wilaya za mkoa, huku akitumia mbinu ya ushawishi na kuwaelimisha hatimaye zoezi la kuwapanga vizuri machinga likafanikiwa.

Kilichofuata ilikuwa ni usafi kwa kuwa maeneo mengi waliyohama yalikuwa machafu ndipo akaandaa muongozo au kitabu ambacho kilibainisha Mkakati wa Usafi na Uhifadhi wa Mazingira katika Mkoa, kukiwa na kauli Mbiu SAFISHA PENDEZESHA DAR ES SALAAM, kampeni ambayo aliizindua rasmi Disemba 4, 2021 akidhamiria kulifanya jiji la Dar es Salaam kuwa Safi wakati wote.

Mambo muhimu yaliyoanishwa kuhusu Kampeni ya Usafi kwanza kabisa Udhibiti wa biashara holela, pili Udhibiti wa Uchafuzi wa mazingira (Utupaji wa taka), Usafishaji wa Jiji/kufanya Usafi, Uzoaji wa Taka zilizozalishwa katika kila mitaa au kata, Usafirishaji wa taka na Uteketezaji, Mkakati wa Upandaji miti,Uendelezaji wa bustani na maeneo ya Umma ya Kupumzika, na ushirikishwaji wa wadau katika kutekeleza mapango.

Mambo hayo ambayo RC Makalla ameyaainisha ikiwa ni mkakati katika Kampeni ya Usafi ndio utekelezaji wake umefanyika na matokeo yameonekana, Wana Dar es Salaam sasa wanapaswa kuendelea kumuunga mkono ili nafasi ambayo jiji kwa sasa limeshika katika usafi lisirudi nyuma badala yake liende mbele zaidi ikiwezekana Jiji la Dar es Salaa liwe la Kwanza Afrika kwa Usafi.

Aidha katika kufurahia ushindi uliopatikana katika kipindi kifupi ni wakati muafaka wa kutafakari na kuijitathimini kwa kuhakikisha hakuna mfanyabiashara anayefanya biashara katika maeneo yasiyo rasmi, kudhibiti utupaji taka ovyo, kufanya usafi iwe ni tabia lakini kila ifikapo tarehe ya mwisho wa mwezi Jamii ijenge utamaduni wa kufanya usafi wa pamoja, kuboresha mzingira ya uzoaji taka zinazozalishwa, usafirishwaji wa taka na uteketezaji katika madampo ya kisasa, vilevile kupanda miti na kuendeleza bustani na maeneo ya Umma ya kupumzika bila kusahau wadau mbalimbali wa mazingira washiriki katika mpango Usafi kwa Ujumla wake.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa