• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla : Kero za Wananchi Wote Kusikilizwa na Kutatuliwa - Kibamba

Posted on: October 31st, 2021

Mhe Amos Makalla akitoa Maelekezo akiwa Jimbo la Kibamba wakati wa muendelezo wa ziara yake ya Jimbo kwa Jimbo kusikiliza na kutatua kero za Wananchi.


-Asema anatembea na Clinic Inayotembea

-Asema KERO kubwa ya MAJI kibamba kuwa historia

-Ataka Ushirikiano Kati ya wananchi na Vyombo vya Ulinzi na Usalama

-Akemea Biashara holela Dar es Salaam

-Asisitiza ushirikishwaji wa Viongozi Ngazi ya Mtaa kabla ya utekelezaji wa Mradi

Hayo yamesemwa Leo tarehe 31 Agosti, 2021 na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla katika muendelezo wa kusikiliza KERO za wananchi katikaJimbo la Kibamba Wilaya ya Ubungo.

*Mhe. Makalla* amesema kuwa ameamua kuwafuata wananchi ili kuwasikiliza na kutatua changamoto walizonazo ambapo anatembea kila Jimbo na "Clinic Inayotembea" yaani akiwa ameongozana na Wataalamu wote wanaohusika." Ofisi yote Imehama ili kuwafuata na kuwahudumia wananchi" Alisema Mhe. Makalla

Akiwa katika Jimbo Hilo Mhe. Mkuu wa Mkoa amepokea KERO mbalimbali ambazo ni pamoja na Kero ya Urasimishaji, ajari nyingi kutokea katika Barabara ya Kimara mpaka Kibaha, tozo kubwa katika Parking za malori, Vituo vya kuuzia mafuta kuondolewa, Migogoro ya Ardhi, na wananchi kuchukuliwa maeneo yao bila fidia.

Kuhusu KERO kubwa inayolikabili Jimbo la Kibamba ya MAJI Mhe. Makalla amesema kuwa Serikali ya awamu ya Sita chini ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan imetenga kiasi cha shilingi billioni 5.4 kwa ajili ya Ujenzi wa Tanki la Kubwa la Mshikamano linaloenda kumaliza tatizo la maji katika Jimbo hilo na litakamilika Juni 2022.

Aidha miradi midogo midogo inaendelea kujengwa na DAWASA ili kuendelea kupunguza shida ya maji.

Wakati huo huo Mhe. Makalla ametaka kuwepo kwa ushirikiano kati ya Wananchi na Vyombo vya Ulinzi na Usalama ambapo amesisitiza kuwa ili wananchi waishi kwa Amani na Utulivu ni vema kuwafichua wahalifu wote waliopo miongoni mwetu.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amekemea pia suala la Biashara holela na kusema hazitakiwa katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Amesema anashangaa kuona utaratibu mbovu wa baadhi ya  wafanyabiashara kuweka Biashara kila sehemu, kuvamia kila upenyo na wengine kupika chakula sehemu hatarishi bila kujali Usalama wao, amesisitiza kuwa hakuna  mfanyabiashara atakayekosa sehemu ya kufanyia biashara Dar es Salaam.

" Tunawafuata wananchi popote walipo ili tuwahudumie na huu ndio Msukumo wa Mhe. Rais". Alisisitiza Mkuu wa Mkoa

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa