• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Azindua Rasmi Kampeni ya Ugawaji Vyandarua na Chanjo ya POLIO

Posted on: April 14th, 2022

-Asema Vyandarua vitagawiwa kwa wanafunzi wa shule ya msingi DSM, takribani 785,548

-Asisitiza watoto wote wenye umri kuanzia miaka 0 - 5 kupatiwa Chanjo ya POLIO

- Atoa Rai juu ya matumizi sahihi ya Vyandarua na Umuhimu wa watoto kupatiwa Chanjo ya POLIO

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Amos Makalla leo April 14 amezindua rasmi Kampeni ya Ugawaji Vyandarua kwa wanafunzi wa shule ya msingi pamoja na Chanjo ya POLIO kwa watoto wenye umri kuanzia 0-5 katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Hafla ya uzinduzi huo imefanyika katika Ukumbi wa mikutano Anatoglo Mnazimmoja Ilala Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Katibu Tawala Mkoa, Sekretarieti ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Viongozi wa Dini, Wawakilishi wa Wazee, Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Wakurugenzi,na Wajumbe wote wa kamati ya huduma za Afya ya Msingi

RC Makalla wakati akizindua Ugawaji wa Vyandarua amesema Vyandarua ni *Salaama vimetengenezwa Tanzania tusipotoshwe, tuvitumie Vyandarua hivyo lakini tusisahau kuchukua tafadhari zote dhidi ya Ugonjwa wa malaria ikiwemo kufanya usafi kuzuia mazalia ya mbu bahati nzuri tayari tuna Kampeni ya Usafi jambo lililoko mbele yetu ni kuendeleza Kampeni hiyo.

Aidha RC Makalla amebainisha kuwa tayari nchi jirani Malawi wamebaini mtu mwenye maambukizi ya Ugonjwa wa POLIO, Tanzania hatuwezi kuwa salama ni vema kuuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuwapatia Chanjo ya POLIO watoto wote wenye umri kuanzia miaka 0-5

Vilevile wananchi waendelee kujipatia chanjo zingine ikiwemo ya Uviko-19 kutokana na ukweli kuwa ukichanja una asilimia kubwa ya kupona ukiugua hivyo "Ujanja ni Kuchanja" Alisema RC Makalla

Kwa upande wa Mganga Mkuu wa Mkoa wa DSM Dkt Rashid Mfaume akitoa taarifa ya awali amesema Kiasi cha Malaria katika Mkoa ni chini ya 1% hali sio mbaya sana lakini ni vyema tukashiriki vizuri katika zoezi la Ugawaji vyandarua kwa wanafunzi na kuhakikisha matumizi sahihi ya vyandarua hivyo.

Kwa upande wa Chanjo ya POLIO watoto watakaopatiwa ni kuanzia umri wa miaka 0-5, hivyo kwa kuwa nchi Jirani Malawi tayari wameshabaini uwepo wa mtu mwenye maambukizi ya POLIO Tanzania lazima tuchukue tafadhari ikiwemo kuwapatia watoto Chanjo hiyo

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Temeke Yang'ara Mwenge wa Uhuru 2025

    June 02, 2025
  • RC Chalamila: Miradi 36 yenye Thamani ya Tsh 79,255,160,719.44 Kupitiwa na Mwenge wa Uhuru Dar

    June 01, 2025
  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa