• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

Posted on: May 16th, 2025

 

-Ni katika kikao Cha Robo ya tatu kati yake na Wakuu wa Sehemu na Vitengo-Mkoa, Wakurugenzi na Wakuu wa Sehemu na Vitengo- Halmashauri

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Toba Nguvila Leo tarehe 15 Mei, 2025 amefanya kikao Cha Robo ya tatu ya mwaka na Wakuu wa Sehemu na Vitengo- Mkoa, Wakurugenzi, Wakuu wa Sehemu na Vitengo- Halmashauri katika Wilaya ya Ubungo ambapo jumla ya maagizo 14 yametolewa naye

Kwanza, amekemea ujenzi wa majengo usiofuata taratibu, ujenzi wa maeneo ambayo hayapaswi kujengwa ambapo wengine  hujenga mpaka ghorofa ndefu na kupelekea kuwachungulia viongozi pia maeneo mengine hayatakiwi maghorofa unakuta yanajengwa hivyo amewaagiza Wakurugenzi, Wahandisi kusimamia taratibu na Sheria za ujenzi na kutokutoa vibali bila Sheria na taratibu za ujenzi kufuatwa

Pili, Dtk. Nguvila amekemea tabia za kumbi za starehe kupiga sana kelele huku zingine kupiga kelele katika  maeneo ya makazi ya viongozi na wananchi kupelekea  kushindwa kupata utulivu hivyo ameagiza Wakurugenzi kulifanyia kazi pia hili

Tatu, Katibu Tawala amewaagiza Wakurugenzi, Maafisa Uchaguzi kuhamasisha wananchiKujiandikisha  kwa wingi kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ambalo kwa Dar es Salaam zoezi la kujiandikisha linatarajiwa kuanza tarehe 16 Mei mpaka 22 ,2025

Nne, RAS Nguvila Amewataka Maafisa Mipango kuwa na Takwimu sahihi vichwani mwao kwani wao ni watu wa kutoa Takwimu hizo mara kwa mara kwenye kazi zao

Tano, Dkt. Nguvila amewaagiza Wakurugenzi kuhakikisha miradi yote isiyokamilika kukamilika na kuanza  kufanya kazi mara Moja, miradi hiyo ya madarasa, Vituo vya afya, na masoko

Sita, Katibu Tawala amewaagiza Wakurugenzi kusimamia Suala la asilimia kumi ipasavyo na kuhakikisha  wanaopata asilimia kumi ni wale makundi lengwa.

Saba, RAS Nguvila amewaagiza Wakurugenzi kusimamia utekelezaji wa Biashara saa 24 na kusema ni jambo linawezekana kabisa kwani limeshaanza kufanya kazi baadhi ya maeneo ya Jiji la Dar es Salaam na kuipongeza Ubungo kwa uzinduzi mkubwa pia

Nane, Katibu Tawala amewaagiza Wakurugenzi kupambana katika kuyainua mapato katika Halmashauri zao huku akitaka malengo ya kukukusanya mapato kutimia  maana vyanzo vya ukusanyaji huo vipo hivyo kuwataka kuongeza watenda kazi

Tisa, Dkt. Nguvila ameeleza Kuhusu Uongezeko la majimbo yaliyopitushwa na  Tume Ya uchaguzi kuwa ni Jimbo la  Chamazi na Kivule hivyo kuwataka Wakurugenzi kuongeza nguvu ya usinamizi

Kumi, RAS Nguvila amewaagiza Wakurugenzi kuongeza usimamizi wa utekelezaji wa Miradi ya kimkakati na katika utekelezaji huo, taarifa za ubia kati yao lazima kwanza zipitie kwa Katibu Tawala kabla ya Kwenda TAMISEMI

Kumi na Moja, Katibu Tawala amewaagiza Wakurugenzi kujiridhisha na miradi itakayopendekezwa kupitiwa na Mwenge wa Uhuru kwani tunajiandaa kukimbiza Mwenge katika Mkoa wetu

Kumi na Mbili Dkt. Nguvila ameeleza uwepo wa mitungi ya Gas ipatayo 1000 kutoka Taifa Gas na kuwaagiza Wakurugenzi ifikapo ijumaa ya wiki ijayo kuichukua na kuwafikishia walengwa

Kumi na Tatu, RAS Nguvila amewaagiza Wakurugenzi kusimamia  matumizi ya Mfumo wa Pepmis na pipmis na kusema ni ya lazima na yeyote asiyetekeleza hili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake

Kumi na Nne,  Katibu Tawala ameagiza madeni ya watumishi na wakandarasi kulipwa na kusema pesa inayokusanywa itengwe na ilipe watumishi na  wakandarasi ili wafanye kazi

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Charles Hilary

    May 13, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa