• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AZINDUA RASMI MRADI WA MAJI WA RUVU JUU MLANDIZI MKOANI PWANI PIA AZINDUA VIWANDA VINGINE MKOANI HUMO JUNI 21, 2017

Posted on: June 21st, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 21 Juni, 2017 amezindua viwanda vikubwa vitatu na mradi wa upanuzi wa mtambo wa maji wa Ruvu Juu na ulazaji wa mabomba makuu kutoka Mlandizi hadi Dar es Salaam ikiwa ni siku yake ya pili ya ziara ya kikazi ya siku 3 mkoani Pwani.

Kwanza, Mhe. Rais Magufuli amezindua kiwanda cha kutengeneza vifungashio cha Global Packaging Tanzania Ltd kilichopo katika eneo la viwanda Kibaha ambacho kina uwezo wa kutengeneza mifuko ya sandarusi 53,000 kwa siku kwa ajili ya kuhifadhia mazao.

Kiwanda hicho kinachomilikiwa na Mtanzania Bw. Joseph Otieno Wasonga kimeajiri watu 110 na kimejengwa kwa gharama ya takribani Shilingi Bilioni 8.

Pili, Mhe. Rais Magufuli amezindua mradi wa kutengeneza matrekta 2,400  aina ya Ursus ambao utagharimu Shilingi Bilioni 55, na matrekta hayo yatasambazwa nchi nzima kwa ajili ya kuboresha sekta ya kilimo.

Mradi huu unamilikiwa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia 100 na utazalisha matrekta ya aina 6 zenye nguvu ya kuanzia HP50 hadi HP 85.

Tatu, Mhe. Rais Magufuli amezindua kiwanda cha chuma cha Kiluwa Steel Group kilichopo Mlandizi ambacho katika awamu hii ya kwanza kina uwezo wa kuzalisha tani 500,000 za nondo kwa mwaka na awamu ya pili kitaongeza uzalishaji hadi kufikia tani 1,200,000 kwa mwaka.

Balozi wa China hapa nchini Mhe. Dkt. Lu Youqing amesema kiwanda hicho kiwanda hicho kinachomilikiwa na Mtanzania Bw. Mohamed Said Kiluwa kwa asilimia 51 na asilimia 49 zinamilikiwa na mwekezaji kutoka China ni muendelezo wa uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati ya China na Tanzania.

Aidha, Shirika la Reli Tanzania (TRL) limejenga njia ya reli ya kilometa 3.5 inayounganisha kiwanda hicho na reli ya kati ikiwa ni juhudi za kurahisisha usafirishaji wa malighafi na vyuma vinavyozalishwa kiwandani hapo kwenda ndani na nje ya nchi.

Akizungumza katika miradi hiyo, Mhe. Rais Magufuli amepongeza uwekezaji huo na ameagiza vyombo vinavyohusika kutoa vibali kwa ajili ya ujenzi wa viwanda hapa nchini viondoe urasimu ambao umekuwa ukiwakatisha tamaa wawekezaji kujenga viwanda.

Mhe. Dkt. Magufuli ametoa wito kwa wamiliki wa viwanda hivyo kujali maslahi na usalama wa wafanyakazi waliowaajiri, amezitaka benki hapa nchini kujielekeza kufanya biashara na wananchi kwa kuwakopesha mitaji wafanyabiashara na wajasiriamali badala ya kutaka kufanya biashara na Serikali na ameiagiza Wizara ya Nishati na madini na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kuhakikisha viwanda vya chuma vinatumia malighafi za hapa nchini kutoka Mchuchuma na Liganga.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amezindua mradi wa upanuzi wa mtambo wa maji wa Ruvu Juu na ulazaji wa mabomba makuu ya maji ya kutoka Mlandizi hadi Dar es Salaam uliojengwa na Serikali ya Tanzania kwa gharama ya Shilingi Bilioni 200 ikiwa ni mkopo kutoka Serikali ya India.

Kabla ya Mhe. Rais Magufuli kuzungumza na wananchi waliohudhuria sherehe za uzinduzi wa mradi huo, Waziri Mkuu wa India Mhe. Nalendra Modi ametoa salamu kwa njia ya luninga ambapo amempongeza Mhe. Rais Magufuli na Serikali yake kwa kufanikisha mradi huo ambao utasaidia kuondoa kero ya uhaba wa maji iliyowakabili wananchi wa Jiji la Dar es Salaam kwa miaka mingi na utaboresha maisha ya watu.

Katika salamu hizo zilizowasilishwa na Balozi wa India hapa nchini Mhe. Sandeep Arya Mhe. Waziri Mkuu Modi ametangaza kuwa Serikali yake imepitisha kiasi cha Dola za Kimarekani Milioni 500 sawa na zaidi ya Shilingi Trilioni 1 ambazo Tanzania itakopeshwa kwa ajili ya kusaidia miradi ya maji katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Waziri Mkuu wa India Mhe. Nalendra Modi kwa kutoa mkopo huo na amesema upanuzi wa mradi wa maji wa Ruvu Juu pamoja na mkopo huo vinaendeleza na kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano mzuri na wa kihistoria kati ya Tanzania na India.

Mhe. Rais Magufuli pia ameitaka Wizara ya Maji na Umwagiliaji kujipanga vizuri kusimamia utekelezaji wa miradi ya maji inayosuasua, kudhibiti upotevu na wizi wa maji na kuwakatia maji wadaiwa sugu wote.

Kesho tarehe 22 Juni, 2017 Mhe. Rais Magufuli atakamilisha ziara yake ya kikazi ya siku 3 Mkoani Pwani kwa kuzindua kiwanda cha vinywaji baridi cha Sayona Drink Ltd, kuzindua kiwanda cha kukausha matunda cha Elven Agric Company na kuzindua mradi wa barabara ya Bagamoyo – Msata.

 

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Kibaha, Pwani

21 Juni, 2017

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Ukatili Kinara Migogoro inayohitaji Msaada wa Kisheria-Waziri Mkuu

    June 16, 2025
  • Wananchi Dar Kunufaika na Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia

    June 14, 2025
  • RC Chalamila, Samia Legal Aid Kuzinduliwa Juni 16, 2025 DSM

    June 13, 2025
  • Wataalam Kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Wakutana na Kamati ya Usalama ya Mkoa-DSM

    June 11, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa