• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Abubakar Kunenge Atembelea Miradi ya Dawasa Iliyopo Katika Mkoa wa Dar es Salaam

Posted on: August 24th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Abubakar Kunenge leo tarehe 24 Agosti, 2020 ametembelea miradi ya DAWASA iliyopo katika Mkoa wa Dar es Salaam ili kuweza kuona utekelezaji wa miradi hiyo yenye lengo la kumtua mama ndoo kichwani.


Awali, Mhe. Mkuu wa Mkoa akiambatana na Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja walianzia katika mradi wa Ujenzi wa Tanki la lita million 15 linalopokea maji kutoka katika visima vya Kimbiji na Mpera lililopo kisarawe 11 lenye thamani ya Shilingi Billioni 30 ambapo litasambaza maji kwenye maeneo ya Wilaya ya Kigamboni.

Baada ya hapo msafara wa Mhe. Mkuu wa Mkoa ulielekea katika mradi wa maji kutoka Kisarawe kuja Pugu Station unaogharimu kiasi cha Shilingi Billion 6.9 ambao utakuwa na uwezo wa kusambaza Lita million 5 kwa Zaidi ya wananchi laki nne wa maeneo ya Chanika, Majohe, Buyuni, Gongo la Mboto, Kigogo na Pugu.

Mhe. Mkuu wa Mkoa pia ametembelea mradi wa Mabwepande mpaka Changanyikeni unaogharimu kiasi cha Shilingi Billioni 67 unaokwenda sambamba na ulazaji wa mabomba ya maji kwa urefu wa km 1700. Huu mradi umefadhiriwa na Benki ya Dunia.

Baada ya kujionea na kupata maelekezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa DAWAS na Wakandarasi wa miradi hiyo Mhe. Kunenge alipata nafasi ya kuongea ambapo aliwapongeza DAWASA kwa utekelezaji wa miradi hiyo mikubwa kwa Mkoa wa Dar es Salaam na kuwataka kukamilisha miradi yote kwa wakati. Aidha, aliwataka kuwafahamisha wananchi kuhusu miradi iliyopo katika maeneo yao. Zaidi aliwataka kuhakikisha upotevu ma maji unazuilika. Vilevile alitumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi nao walipe bili zao inavyotakiwa na kwa wakati.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja aliwahakikishia wananchi wa Dar es Salaam kuwa shida ya maji sasa inakwenda kuisha.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa