• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI

Posted on: July 11th, 2017

MHE.PAUL MAKONDA AMEWEKA JIWE LA MSINGI KATIKA JENGO LA DHARURA HOSPITALI YA TEMEKE

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mheshimiwa Paul C. Makonda leo ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la kisasa la huduma za dharura (EMERGENCY BLOCK) Hospitali ya Temeke ambalo ujenzi wake utagharimu zaidi ya shilingi Million 800 linalofadhiliwa na ubalozi wa Japan Nchini Tanzania.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo Mheshimiwa Makonda amesema jengo hilo litakuwa na uwezo wa kusaidia zaidi ya watu 2000 kwa siku ambapo litakuwa na chumba cha upasuaji, chumba cha ICU, vyumba vya uangalizi maalumu wa wagonjwa pamoja na vyumba vya madaktari.

Aidha jengo hilo litakuwa na vyumba maalumu vya watoto (njiti), Kinamama na Wababa ambapo lengo ni kuhakikisha Mgonjwa yoyote wa Dharura iwe wa Ajali, Upasuaji kwa kinamama Wajawaziito,Malaria ya ghafla, Moto na wanaobanwa na Kifua wanapatiwa huduma ya haraka ambapo kwa hatua hiyo itasaidia kupunguza mlundikano wa Wagonjwa wa dharura Hospital ya Taifa Muhimbili kama Rais Dkt.Magufuli anavyotaka.

“Mimi nimeshuhudia watu wengi wakipoteza maisha kwa kukosa huduma za dharura, hii ndio iliyonisukuma kutafuta kila njia ili wananchi wangu wasipoteze maisha kwa sababu tu ya kukosa huduma ya haraka, nikaamua kumtafuta balozi wa Japani na kumshirikisha jambao hili, Balozi aliponisikiliza na kunielewa akakubali kuniunga mkono katika mapambano yangu ya kuboresha huduma za afya kwa wananchi hasa wanyonge na ameshanipa fedha kwaajili ya ujenzi wa jengo hilo na hivi tunavyoongea tayari mkandarasi ameanza na ujenzi” Alisema Makonda.

Aidha Mheshimiwa Makonda amesema kuwa ujenzi wa jengo hilo utachukuwa miezi sita hadi kukamilika na kueleza kuwa dhamira yake ni kuhakikisha Dar es salaam inakuwa Mkoa unaotoa huduma bora za Afya.

“Watu hatukumbukwi kwa maneno bali kazi tulizofanya. Kwa kuwa Rais Magufuli amenipa Mkoa niongoze na mimi ni lazima nitumie akili na kipaji ambacho Mungu amenipa kutatua Changamoto za Afya katika Mkoa wangu” Aliongeza Makonda.

Kwa upande Mwakilishi wa Balozi wa Japani Nchini Tanzania Bwana Hiroyuki Kubota amesema serikali ya Japan itaendelea kushirikiana na Tanzania katika masuala mbalimbali huku Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mheshimiwa Felix Lyaniva akimpongeza Makonda kwa namna anavyopambana kutatua kero za Wananchi.


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa