• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

KATIBU TAWALA WA MKOA NDG ABDUL MHINTE ATAKA MAARIFA ZAIDI YATUMIKE KATIKA UKUSANYAJI WA MAPATO DSM

Posted on: September 10th, 2025

 

-Apongeza Jitihada zinazofanywa na Halmashauri ya Jiji na Manispaa ya Kinondoni katika ukusanyaji wa mapato

-Asisitiza ubunifu na matumizi ya Teknolojia katika shughuli za ndani ya ofisi, ukusanyaji wa mapato na katika kuwahudumia wananchi

-Atoa Rai kujitokeza kwa wingi kupiga kura uchaguzi mkuu Oktoba 29,2025

-Ataka kutolewa elimu zaidi kwa umma namna bora ya kuishi mjini (usafi)

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Ndg Abdul Rajab Mhinte amewataka wataalamu katika Mkoa huo kutumia zaidi maarifa kuliko nguvu katika ukusanyaji wa mapato.

Ameyasema hayo leo Septemba 10, 2025 kwa nyakati tofauti akiwa anaongea na watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.

Katibu Tawala Mhinte amepongeza kwa ujumla jitihada zinazofanywa na Halmashauri hizo katika ukusanyaji wa mapato ambapo amezitaka kuongeza jitihada zaidi kwa kuwa Dar es Salaam  ni jiji kubwa na lina vyanzo vingi vya mapato.

Aidha amesisitiza matumizi ya maarifa zaidi kuliko nguvu, hivyo amewataka kuwa wabunifu, matumizi ya teknolojia katika shughuli za kila siku ndani ya ofisi  na katika kuwahudumia wananchi hivyo "Ningefurahi zaidi kero nyingi za wananchi zitatuliwe katika ngazi za chini, pia wananchi wahudumiwe vizuri, lugha yenye staha itumike" Alisema Ndg Mhinte.

Sambamba na hilo Katibu Tawala amezitaka Halmashauri hizo kuwa na programu mbalimbali za elimu kwa umma hususani masuala yahusuyo usafi katika Jiji ambapo amesema wananchi waelimishwe namna nzuri ya kuishi mjini pia ametoa rai kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura Octoba 29, 2025 katika uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji Ndg Elhuruma Mabelya na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Bi Hanifa Hamza kwa niaba ya watumishi wemeahidi kuyafanyia kazi maagizo yote ya Katiba Tawala wa Mkoa pamoja na kuwa wabunifu zaidi katika nyanja mbalimbali kwa masilahi mapana ya wananchi wa Halmashauri hizo na Taifa kwa ujumla.

Ifahamike kuwa Katibu Tawala wa Mkoa Ndg Abdul Rajab Mhinte yuko katika ziara ya kujitambulisha katika Halmashauri zote za Mkoa huo toka apate uteuzi wa kuhudumu katika Mkoa huo ambapo Septemba 11,2025 anatarajia kukutana na watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke na Kigamboni

Matangazo

  • DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050 July 17, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA WA DARASA LA SABA MEI, 2025 July 18, 2025
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KATIBU TAWALA WA MKOA DSM NDG ABDUL MHINTE AKUTANA NA WATUMISHI WA WILAYA YA TEMEKE NA KIGAMBONI

    September 11, 2025
  • KATIBU TAWALA WA MKOA NDG ABDUL MHINTE ATAKA MAARIFA ZAIDI YATUMIKE KATIKA UKUSANYAJI WA MAPATO DSM

    September 10, 2025
  • Katibu Tawala wa Mkoa na Madaktari wasio na Mipaka Wasaini Makubaliano ya Usaidizi Utoaji Huduma za Dharula.

    September 03, 2025
  • Tukio la kusaini Mkataba wa Makubaliano ya Mashirikiano kati ya Water Aid na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Halmashauri ya Jiji , Kigamboni na Temeke.

    August 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa