• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

GAIN Kuwezesha Soko la Buguruni Kuendelea na Uzalishaji katika hali ya Usalama

Posted on: February 2nd, 2022

Shirika la GAIN kupitia mradi wa kuwezesha masoko kuzalisha katika hali ya Usalama KFMW leo  wamefanya kikao na Wadau katika Ukumbi wa Lecam Social Hall Buguruni Ilala- Dar es Salaam.

Akiongea wakati wa Kikao hicho Meneja wa mradi Ndg Edwin Josiah amesema Kikao kilikuwa na lengo la kuwasilisha matokeo ya tafiti zilizofanyika juu ya mtazamo wa wauzaji na wanunuzi katika masoko hususani Soko la Buguruni kuhusu Usalama wa Chakula ( Safe food ) Sokoni.

Aidha Bwana Edwin amefafanua kabla ya kikao hicho wamepata wasaa wa kutembelea na kujionea Uhalisia kwa sasa katika Soko la Buguruni na kuongea na wafanyabiashara kusikia maoni na ushauri, hivyo kikao kilichofanyika kimetoa fursa kwa wadau kwa pamoja kujadili namna bora ili kufikia adhima ya Usalama wa Chakula katika Masoko likiwemo Soko hilo.

Kwa upande wa Meneja wa Soko hilo Ndg Seleman mfinanga amesema Shirika la GAIN wamekua mdau mzuri katika kufikia Usalama wa Chakula katika Soko la Buguruni kwa kufadhiri Ukarabati mkubwa wa Soko kuanzia kuweka Sakafu, kuezeka paa sehemu ya kina mama lishe, Kuboresha sehemu ya mchinjio ya kuku, Kuwapa majiko ya gesi kwa kina mama lishe ili waachane na matumizi ya mkaa, hapo awali Soko lilikuwa katika hali isiyofaa kwa Usalama wa Chakula kulikuwa na tope Kipindi cha mvua, vibanda havikuezekwa lakini kwa sasa Soko liko katika Mazingira mazuri hivyo tunawashukuru sana Shirika la GAIN

Mwisho Kikao kazi hicho kimehudhuliwa na Wataalam toka Wizarani ,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Ofisini ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala ,Viongozi wa Soko la Buguruni, wafanyabiashara na Wataalam kutoka Shirika la GAIN ( Global Alliance for Improved food Nutrition)


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Waombolezaji Kuaga Mwili wa Charles Hilary

    May 13, 2025
  • Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa yakagua Miradi ya Maendeleo Wilaya ya Temeke

    May 07, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Maadhimisho ya Mei-Mosi Dar es Salaam.

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa