• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Biashara
    • Utalii
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

Maliasili na Mazingira

MALIASILI NA MISITU

Eneo la hifadhi ya misitu la Mkoa kwa sasa ni Ha 4199 kwa mwaka huu 2017 , Ha.3,697 mwaka 2008 ambapo mwaka 2005 ilikuwa ha.588 na mwaka 2000 ha.90 tu. Ongezeko hili linaonyesha kuwa jitihada za kuongeza hifadhi ya misitu katika Mkoa ni kubwa na za kuridhisha.

Kuhusu upandaji miti, Mkoa unaendelea kuwaelimisha na kuwahimiza wadau mbalimbali kupanda na kuitunza miti katika maeneo yao. Katika kuimarisha zoezi hili tarehe 01/10/2016 Mkoa umezindua kampeni ya upandaji miti ijulikanayo kama MTI WANGU. Katika kampeni hii Wananchi katika ngazi ya Kaya wanahimizwa kupanda miti isiyopungua 5 ya matunda na kivuli. Kupitia kampeni hii Mkoa umepanga kupanda miti milioni 4 kufikia mwaka 2019 ili kuboresha mazingira ya Jiji kwa kuongeza Ukanda wa Kijani na kupendezesha Jiji (City greening and beutification). Aidha katika utaratibu huu aina ya miti mbalimbali hupandwa kila mwaka ikiwamo ya matunda, mapambo nishati na biashara. Maeneo yanayopandwa miti ni:- maeno ya wazi, barabara, makazi, taasisi mbalimbali, viwandani, kandokando ya mito, mabondeni, fukwe za bahari na maeneo ya vyanzo vya maji.


SIKU YA UPANDAJI MITI KITAIFA

Kila ifikapo tarehe 01 Aprili ya kila mwaka ni Siku ya Upandaji miti Kitaifa. Mkoa wa Dar es Salaam hufanya maadhimisho haya katika ngazi ya Mkoa. huadhimishwa katika moja ya wilaya kwa mzunguko/zamu kwa kila mwaka ambapo wadau wote hushiriki kwa kupanda miti katika maeneo mbalimbali.

Mwaka 2016/2017 sherehe hizo zilifanyika katika wilaya ya Ilala kata ya Msongola, Shule ya Msingi Yangeyange ambapo jumla ya miti 3000 ya Mijohoro, Miembe, Miharadani na Palm ilipandwa katika siku hiyo ya maadhimisho. Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Sophia Mjema.


(a) UTEKELEZAJI WA UPANDAJI MITI MSIMU 2016/2017

Lengo la Mkoa lilikuwa ni kupanda miti 1,000,000 kwa kuzingatia utekelezaji wa kampeni ya MTI WANGU ya kupanda miti 4,000,000 kuanzia mwaka 2016 hadi kufikia mwaka 2019 ambapo Manispaa ya Ilala ilipanda miti 16158, Kigamboni 5116, Kinondoni 20,633, Temeke 13,948, Ubungo 14,372. Utekelezaji halisi jumla ya miti 70,227 ilipandwa kimkoa. Mwaka 2015-2016 jumla ya miti 30,473 ilipandwa ambapo Manispaa ya Ilala ilipanda miti 2822, Kinondoni 9100, Temeke 18,557.

Utekelezaji huu wa upandaji miti kimkoa kuanzia 2015/2016, na 2016/2017, jumla ya miti 100,700 imepandwa katika mkoa wa Dar es Salaam.

  • TAKWIMU MBALIMBALI ZA MALIASILI NA MAZINGIRA KATIKA MKOA WA DAR ES SALAAM.

 

  • IDADI YA VITALU VYA MICHE NA MITI VILIVYOPOI:

 

Halmashauri
Idadi ya vitalu
Mahali
Maelezo
Ilala
2
Kinyamwezi gargden – 1.
Kitalu cha mboga, miche ya miti na matunda.
Karimjee botanical garden - 1
Kitalu cha miche ya miti na maua.
Kigamboni
1
Gazaulole
Kitalu cha mboga na miche ya matunda
Kinondoni
Hakuna

Vilivyopo 3 vimebinafsishwa kwa matumizi mengine ya maeneo hayo. Kitalu kimoja kitaanzishwa katika bustani ya Boko kwa msimu wa 2008/2009.
Temeke
2
Mtoni kwa Azizi Ali garden - 1
Kitalu cha miche ya miti, matunda na maua.
Temeke
1
Ofisi ya Wakala wa huduma za misitu veta
Kinamilikiwa na wizara ya maliasili na utalii
Ubungo
hakuna

Wamepanga kuanzisha ki
Jumla
5
 
 

 

  • HIFADHI YA MISITU ILIYOPO.

Halmashauri

Aina

Eneo (Ha)

Mahali

Maelezo

Kinondoni
(Miombo) Msitu wa asili wa hifadhi ya pori la akiba la Pande (Pande game reserve)
1,223
Mabwe Pande
Unasimamiwa na Wizara ya maliasili/Utalii.
Shamba la miti la Manispaa (msitu wa kupandwa).
5
Bunju B
Unatunzwa na kikundi cha mazingira Bunju.

Hifadhi ya misitu ya Mikoko).
189.5
Kata za Mbweni, Kunduchi,Ununio, Msasani na Kawe.
Inasimamiwa na Wizara ya Maliasili- Idara ya misitu kitengo cha mikoko ikisaidiana na Halmashauri ya Manispaa, CBO`s na vikundi vya mazingira.
Misitu ya Kupandwa (watu binafsi).
45
Mabwe Pande na maeneo mbalimbali.
Inamilikiwa na kusimamiwa na watu binafsi.
Jumla
1,462.5


Kigamboni
Shamba la miti la Manispaa
13.6
Kata ya Kimbiji na Toangoma.
Linasimamiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.
Misitu ya kupandwa (watu binafsi)
25
Kata ya Somangila na Kimbiji.
Husimamiwa na kumilikiwa na watu binafsi.
Misitu ya mikoko.
2,500
Maeneo ya fukwe za bahari.
Inasimamiwa na wizara ya Maliasili – Idara ya Misitu Kitengo cha ikoko ikisaidina na Halmashauri ya Manispaa, CBO`s  na vikundi vya mazingira.
Misitu ya asili
36
Kata ya Amani gomvu na Somangila
Watu binafsi.
Jumla ndogo

2574.6


Temeke
Mikoko

13.2

Kata ya Mtoni kijichi
Unasimamiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii
Mikoko

8.3

kurasini
Unasimamiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii
Mikoko

7

kizinga
Unasimamiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii
Jumla Ndogo

28.5



Ilala
Misitu ya asili.
13
Kitunda
Watu binafsi.
Shamba la  Manispaa
5
Kinyerezi
LInasimamwia na Manispaa.
Msitu wa mikoko
10
Daraja la Salenda
Inasimamiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kwakushirikiana na Manispaa
Hifadhi ya msitu wa asili wa Zingiziwa.
105
Chanika
Linasimamiwa na Manispaa na vikundi vya utunzaji mazingira.
Jumla ndogo

133



Jumla
Mikoko
2728


Jumla
Misitu ya kupandwa
75


Jumla
Misitu ya asili
1,395.6


Jumla ya eneo la misitu yote 
4199
 
 

 

Matangazo

  • FOMU YA KUHUISHA MAJUKWAA YA KUWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI DSM November 09, 2022
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Ratiba ya Mtihani wa Kumaliza Kidato cha Sita (ACSEE) - 2020 June 12, 2020
  • Matokeo ya Uchaguzi wa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 Shule za Sekondari za Serikali December 18, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Makalla Masoko Mapya Yatakayojengwa Washirikishwe Machinga na Viongozi wa Soko

    March 11, 2023
  • RC Makalla Aeleza Kishindo Cha Rais Dkt Samia Suluhu Miaka 2 DSM

    March 10, 2023
  • RC Makalla Atimiza ahadi ya Kuwapeleka Viongozi wa Machinga Taifa Kigali Rwanda

    March 10, 2023
  • RC Makalla Hakuna Fremu Soko la Kariakoo Zilizogawiwa Epukeni Matapeli

    March 26, 2023
  • Tazama zote

Video

RC Makalla akikagua Maendeleo ya Ujenzi na ukarabati wa Soko la Kariakoo
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa