• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Atoa Maelekezo Matano kwa Wenyeviti na Watendaji wa Kata na Mitaa

Posted on: June 20th, 2022

 .

- Ataka usimamizi madhubuti wa Operesheni ya anuani za Makazi na Sensa.

- Aelekeza Agenda ya Ulinzi na usalama ipewe kipaombele kuanzia ngazi ya Mtaa.

- Asisitiza Udhibiti wa Biashara holela na Usafi.

- Watendaji wamuahidi kusimamia utekelezaji wa maelekezo hayo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla leo amefanya kikao kazi Cha maelekezo na Viongozi wa ngazi ya Wilaya, Kata na Mitaa wakiwemo Madiwani, Wenyeviti wa Mitaa na  Watendaji wa Kata/ Mitaa na kuwapatia maelekezo matano ya kutekeleza.

Miongoni mwa maelekezo hayo ni pamoja na Usimamizi madhubuti wa Operesheni ya anuani za Makazi ambapo amesema kwa Mkoa huo ni lazima zoezi Hilo lifanyike kwa ukubwa kwakuwa Dar es salaam ndio uso wa Nchi.

Aidha RC Makalla amewapongeza Viongozi na Wananchi kwa ushirikiano mkubwa walioonyesha kufanikisha awamu ya kwanza na kufanya Mkoa Kuvuka lengo kwa Asilimia 104 ambapo ameelekeza awamu hii ya pili ya uwekaji Nguzo kwenye Barabara, Mitaa na Vibao kwenye Nyumba kufanyika kwa Kasi na ufanisi.

Aidha RC Makalla amewataka Watendaji hao kuhakikisha Ifikapo August 23 kila Mwananchi anahesabiwa kwenye zoezi la Sensa ya watu na Makazi ili kuwezesha Serikali kujua idadi ya Wananchi na kuweza kupanga Bajeti na namna ya kutoa huduma.

Katika kikao kazi hicho, RC Makalla amewapongeza Wenyeviti wa Mitaa kwa kufanikisha Operesheni tokomeza Panya road jambo lililopelekea Jiji kuwa shwari ambapo ameelekeza agenda ya Ulinzi na usalama kuwa agenda ya kudumu kwenye vikao na mikutano.

Hata hivyo RC Makalla ameendelea kusisitiza Watendaji hao kudhibiti suala la Ufanyaji Biashara holela kwenye maeneo yaliyokatazwa ambapo amesema Mtendaji atakaeonekana kulegalega kwenye usimamizi atakuwa anapoteza sifa ya kuongoza eneo alilopo.

Kuhusu suala la Usafi RC Makalla ameelekeza Usimamizi wa Kampeni ya SAFISHA PENDEZESHA DAR ES SALAAM kwa kuhakikisha Wananchi wanafanya Usafi kila Jumamos na Usafi wa pamoja kila Jumamos ya mwisho wa Mwezi.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa