• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Chalamila Vyombo vya Habari ni Muhimili Muhimu kwa Taifa

Posted on: December 5th, 2025

 

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila amewataka wahariri na waandishi wa habari kufanya kazi yao bila upotoshaji wa taarifa hususani kwenye masuala yanayoweza kuleta taharuki kwenye jamii na kusisitiza kuwa Serikali Mkoani humo haikubaliani na matukio ya ya uhalifu ikiwemo utekaji.

Akizungumza katika mkutano na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari jijini Dar es salaam leo Disemba 5, 2025 RC Chalamila amesema upotoshaji wa taarifa unaweza kuligharimu Taifa hasa nyakati zenye taharuki huku akitolea mfano wa matukio ya uchaguzi mkuu wa oktoba 29 ambapo ameeleza wazi kuwa Serikali imejipanga vyema kukabiliana na vitendo vya uhalifu ikiwemo utekaji.

Aidha RC Chalamila amesema Serikali inaendelea kuzifanyia kazi changamoto za makundi yote ndani ya jamii ikiwemo vijana hivyo ni muhimu kuondoa taharuki kwenye jamii kwani Serikali imepokea changamoto za makundi yote

Vilevile RC Chalamila ametumia Mkutano huo kuwataka wahariri,wanahabari na jamii kwa ujumla kuiamini tume iliuoundwa na Rais Dkt Samia na kusubiri matokeo sahihi yatokanayo na tume hiyo badala ya kila mtu kutoa taarifa akitumia fikra zake akiwa kwenye taharuki huku pia akiitaka jamii kujielekeza kwenye hoja ya maridhiano ili kijua nini kinahitaji kuboreshwa

Kwa upande wake Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Jumanne Muliro amezungumzia majukumu ya jeshi la polisi na uwepo wa mipaka ya kiutendaji kwa kila kundi ili kuimarisha amani na amesisitiza kuwa jishi hilo litaendelea kushirikiana na waandishi wa habari huku akiiasa jamii kutoshabikia vurugu na uvunjifu wa amani

Hata hivyo Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri nchini TEF Deodatus Balile amesema wao kama wahariri wanatambua umuhimu wa uwepo wa amani na wapo tayari kushiriki kikamilifu kudumisha amani ya nchi na kusisitiza uandishi uliojikita kwenye ukweli licha ya uwepo wa viashiria vya uvunjifu wa amani huku mmoja wa wahariri na Mwanahabari mkongwe Absalom Kibanda akisisitiza kuwa wanahabari wanapaswa kufanya kazi kwa uhalisia na sio kusukumwa na hisia na ushabiki na amesisitiza Jeshi la Polisi kushirikiana na wanahabari wakati wa vurugu

Naye Joyce Shebe ni mmoja wa wahariri waliopata fursa ya kutoa maoni ambapo amesisitiza kuwa ni muhimu kwa serikali kuweka mazingira bora kwa wanahabari kufanya kazi pia wanahabari kufanya kazi za uchunguzi kuhamasisha amani pamoja na kufafanua habari zenye maslahi mapana kwa jamii

Matangazo

  • MWENENDO WA BEI WIKI YA 24-28 NOVEMBA 20225 DAR ES SALAAM December 01, 2025
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Vyombo vya Habari ni Muhimili Muhimu kwa Taifa

    December 05, 2025
  • RC Chalamila Azindua Wodi ya Watoto Wachanga Hospitali ya Amana

    December 03, 2025
  • Rais Dkt Samia Suluhu Akutana na Wazee wa Dar es Salaam

    December 02, 2025
  • Rais DKT Samia Kuzungumza na Wazee wa Dar Disemba 2,2025

    December 01, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa