• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

Hali ya Utoaji Huduma ya Majisafi,Uondoaji Majitaka na Mipango Iliyopo na Miradi Inayoendelea, Mkoa wa Dar es Salaam Hadi Juni, 2018

Start Date: 2018-06-30
End Date: 2018-12-31

HALI YA UTOAJI HUDUMA YA MAJISAFI, UONDOAJI MAJITAKA NA

MIPANGO ILIYOPO NA MIRADI INAYOEENDELEA

MKOA WA DAR ES SALAAM 

 HADI JUNI, 2018

HUDUMA YA MAJI 

 

  • 1.1 Hali ya Upatikanaji wa Huduma ya Maji

Mahitaji ya maji kwa wakazi wa Dar es Salaam hadi  mwezi Juni,  2018 ni wastani wa lita milioni 544 kwa siku ambapo uwezo wa uzalishaji ni lita milioni 502 kwa siku. Vyanzo vikuu vya maji haya ni Mto Ruvu (88%), Mto Kizinga (03%) na visima virefu (09%). Maji yanayozalishwa kwa sasa yanakidhi mahitaji kwa  asilimia 75 ya wakazi wa Jiji. Takriban asilimia 40 ya eneo la Mkoa halina mtandao wa mabomba ya DAWASA ambapo huduma hupatikana kupitia Visima vya Taasisi na watu binafsi, huduma hii huchangia asilimia 16 ya mahitaji.

Maeneo machache (20%) yaliyopo hasa katika Wilaya ya Kinondoni, Ilala na Ubungo hupata huduma ya maji kwa saa kati ya 20-24 wakati zaidi ya asilimia 40 hupata maji kwa mgawo wa wastani wa saa kati ya 8-16 kwa siku.

Eneo kubwa la Wilaya za Temeke na Kigamboni ndilo lenye kiwango cha chini ya asilimia 10 ya upatikanaji wa mtandao wa mabomba. Maeneo haya yanatarajiwa kupata huduma ya maji kutoka mradi mkubwa unaoendelea hivi sasa wa visima virefu 20 vya Kimbiji na Mpera

Jitihada za kuongeza mtandao wa Majisafi zinaendelea ili watu wengi zaidi waweze kunufaika. Hadi kufikia mwezi Juni, 2018 asilimia 75 ya wakazi waishio kwenye Mitaa katika Mkoa wa Dar es Salaam wanapata huduma ya majisafi na salama kupitia miradi ya maji iliyopo.

1.2      Hali ya Uondoshaji Majitaka Mkoa wa Dar es Salaam

Mfumo (Central sewerage system) wa kuondosha Majitaka uliopo Jijini Dar es Salaam unahudumia asilimia 10 tu ya wakazi wote wa Jiji. Mifumo mingine ipo Lugalo, Chuo Kikuu cha DSM, Mwenge, Kijitonyama, Mikocheni, Kurasini, Buguruni, Uwanja wa Ndege, Airwing, Barabara ya Nyerere (Tazara), Vingunguti na Ubungo. Mifumo hii inamwaga majitaka katika mabwawa yaliyoko maeneo hayo.

Maeneo yasiyo na mfumo rasmi wanatumia vyoo vya shimo (Pit latrine) asilimia 70 na mashimo ya choo (septic tanks) asilimia 20.

Matarajio ya Mkoa ni kutoa huduma ya Majisafi na salama kwa asilimia 95 ya wakazi wa Jiji na asilimia 30 uondoshaji wa Majitaka katika Mkoa wa Dar es Salaam ifikapo 2025.

  • 1.3 Mpango wa Kuongeza Upatikanaji wa Huduma ya Maji katika Mkoa wa Dar Es Salaam
  •  1.3.1 Mipango Kupitia Programu ya Maendeleo ya Sekya ya Maji (WSDP) inayotekelezwa na Halmashauri za Manispaa.

Hivi sasa Mkoa wa Dar es Salaam unaendelea kutekeleza jumla ya miradi 18 kati ya 41 ya visima vya maji iliyopangwa, katika Manispaa ya Ilala, Kigamboni, Kinondoni, Temeke na Ubungo chini ya mpango wa Maendeleo wa Sekta ya Maji. Kati ya miradi hiyo, 10 imekamilika na inatoa huduma kwa wananchi (Pugu Kajiungeni, Kipunguni B, Makongo Mbuyuni, Kivule, Goroka, Mianzini, Kizinga Bughidad, Mashine ya Maji, Kibwegere na Mpiji-Magohe). Aidha, miradi 3 ya Mbuyuni, Mamboleo B na Mabatini ipo katika hatua ya majaribio ya utoaji wa huduma ya maji. Kazi za utekelezaji wa miradi 5 ya maji ya Chambewa, Kibene, Malimbika, Kizuiani na Mbezi Makabe zinaendelea.

Katika kuhakikisha miradi ya maji inakuwa endelevu, miradi yote inaendeshwa na wananchi wenyewe kupitia Vyombo vya Watumiaji Maji/Vikundi vinavyoundwa kisheria. Aidha, miradi ambayo inatumia mtandao wa DAWASA uendeshaji wake unakuwa chini ya DAWASCO.

1.3.2    Miradi Mingine inayotekelezwa kwenye Halmashauri

Kupitia bajeti za Halmashauri (Own Source, UNICEF, LGCGD, BTC, WATER AID, Africa Relief, Food Aid Counterpart na mfuko wa Jimbo) Halmashauri zote tano zinaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maji katika maeneo yao kama ifuatavyo:-

Manispaa ya Ilala

Katika Manispaa ya Ilala, jumla ya Miradi 10 inatekelezwa katika maeneo ya Pugu Bangulo, Kinyerezi, Pugu Kichangani, Ulongoni A, Lada, Lubakaya, Lukooni, Segerea, Kitonga. Upanuzi wa mradi wa usambazaji wa maji katika maeneo ya Kinyamwezi, Mustafa na Viwege ujenzi wake umekamilika. Wananchi 27,064 wananufaika na huduma ya maji inayotolewa katika maeneo hayo. Aidha, Mradi wa maji katika mtaa wa Mkera ujenzi wake unaendelea na umefika asilimia 90.

Manispaa ya Kigamboni

Manispaa ya Kigamboni kuna jumla ya Miradi 2, mradi wa Mwasonga-Kisarawe II ujenzi wake umekamilika na umeanza kutoa huduma ya majaribio na Minondo Somangila ambao ujenzi umesimama kwa muda kupitisha nguzo za umeme.

Manispaa ya Kinondoni

Jumla ya Miradi 3 ya Makongo Juu, Kigogo Buyuni na Shule ya Msingi Changanyikeni imekamilika. Wananchi 7,017 wananufaika na huduma ya maji inayotolewa.

Mradi wa maji wa Mivumoni ukarabati wake unaendelea, ununuzi wa Pampu mpya unahitajika baada ya ile ya awali kuharibika.

Manispaa ya Temeke

Manispaa ya Temeke, jumla ya Miradi 3 ya Kurasini-Mvinjeni, Buza na Makuka ujenzi wake umekamilika na imeanza kutoa huduma ya maji. Wananachi zaidi ya 7000 wananufaika na mradi

Mradi wa uboreshaji wa huduma ya maji katika kata tatu maeneo ya Kibondemaji unaotekelezwa kwa msaada wa Shirika la Water Aid/PDF ujenzi wake umekamilika na umeanza kutoa huduma kwa jamii. Mradi unahudumia Wananchi 19,500.

Mradi wa Maji wa Mkondogwa unaendelea na ujenzi wake upo hatua za mwisho za ukamilishaji.

Ujenzi wa mfumo wa kutibu Majitaka (DEWATs) katika eneo la Toangoma unaotekelezwa kwa msaada wa Shirika la Water Aid/PDF, ujenzi wake unaendelea ambapo hadi sasa umefikia 98%, kazi zilizobaki ni ujenzi wa fensi na kusawazisha eneo.

Manispaa ya Ubungo

Jumla ya Miradi 4 ya Makurumla mnara wa Voda, Makurumula Sisi kwa Sisi, Nzasa A na King'azi imekamilika na inatoa huduma kwa Wananchi 11,100.

Upanuzi wa mradi wa King’azi A unaendelea, ukihusisha ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji lenye ujazo wa uwezo wa lita 90,000 litakalohudumia wakazi wapatao 15,400. Hadi sasa utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 40.

Ujenzi wa mfumo wa kutibu Majitaka (DEWATs) katika eneo la Mburahati/ Barafu, umefikia asilimia 60 ya utekelezaji.

Maelezo ya kina kuhusu mipango iliyopo na miradi mbalimbali inayoendelea yanapatikana kwenye Jedwali Na I.

1.3.3 Miradi Inayoteekelezwa na DAWASA

i)Upanuzi wa Mtambo wa Ruvu Chini na ujenzi wa bomba kuu kutoka Ruvu Chini hadi matanki ya Chuo Kikuu cha Ardhi.

 Lengo la mradi huu ni kuongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 182 hadi 270 kwa siku. Mradi wa upanuzi wa mtambo umekamilika kwa asilimia 100 na unatoa huduma. Mradi huu umepunguza kero ya maji kwa wakazi wa maeneo ya Bunju, Mabwepande, Boko, Tegeta, Kunduchi, Mbezi Beach, Mbezi Juu, Salasala, Kawe, Makongo, Chuo Kikuu, Mikocheni, Msasani, Masaki, Mwananyamala, Kinondoni, Magomeni, Sinza, Manzese, Ubungo, Mabibo, Kigogo, Buguruni, Ilala, Maeneo ya Katikati ya Jiji la DSM pamoja na Kurasini, Keko, Chang'ombe, Pugu Road na Bandarini.

ii) Upanuzi wa chanzo cha Ruvu Juu na ujenzi wa bomba kuu hadi matanki ya Kibamba na Kimara.

Lengo la mradi huu ni kuongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 82 hadi 196 kwa siku. Upanuzi wa mtambo umekamilika kwa asilimia 100. Kukamilika kwa mradi huu kumepunguza kero na uhaba wa maji katika maeneo Kiluvya, Kibamba, Changanyikeni, Ubungo, Mbezi, Makabe, Msakuzi, Malamba Mawili, Matosa, Kimara, Kibangu, Makuburi, Tabata, Segerea,  Kinyerezi, Vingunguti,  Airport,  Ukonga,  Kipawa na katikati ya Jiji la DSM. 

iii)Mradi wa visima virefu 20 Kimbiji na Mpera na Uchimbaji wa Visima vya Majaribio.

Lengo la mradi ni kuzalisha lita milioni 260 za maji kwa siku. Kazi ya uchimbaji visima 19 kati ya 20 unaendelea ambapo visima 14 vimechimbwa hadi mwisho, wakati visima 05 uchimbaji wake unaendelea.

Visima vya maeneo ya Mpera vitahudumia wakazi wa maeneo ya Gongo la Mboto, Chanika, Luzando, Pugu, Mpera, Chamazi, Kitunda, Ukonga, Kinyerezi, na Uwanja wa Ndege;

Visima vya maeneo ya Kimbiji vitahudumia wakazi wa maeneo ya Temeke, Kisarawe, Kibada, Kimbiji, Kigamboni, Tuangoma, Mkuranga, Kongowe, Mbagala, Kurasini, Mtoni, Tandika, Keko na Chang’ombe. Mradi wa uchimbaji visima unaendelea na unatarajiwa kukamilika mwaka huu 2018. Aidha, Mradi wa uendelelezaji mradi huu upo katika hatua za majadiliano.

Mradi wa Upanuzi wa Mfumo wa Kusambaza majisafi.

Lengo la mradi ni kuongeza mfumo wa usambazaji maji na kuunganisha wateja wote walioko katika maeneo yasiyo na mtandao na yale yatakayopata maji kutokana na upanuzi wa mitambo ya Ruvu Chini na Ruvu Juu, pia maeneo yatakayopata maji ya visima vya Kimbiji na Mpera. Mradi huu unaendelea kwa maeneo yanayopata maji kutoka mitambo ya Ruvu. Maelezo ya kina kuhusu mipango iliyopo na miradi mbalimbali inayoendelea yanapatikana kwenye Jedwali Na II.

2.0 MAFANIKIO

Kukamilika kwa Mradi Mkubwa wa Ruvu Chini ambao umeongeza upatikanaji wa Maji kutoka Lita Milioni 182 na kufikia lita milioni 270. Mradi umekamilika Mwezi Machi, 2016 na unatoa huduma ya maji kwa Wananchi;

Kukamilika kwa Mradi Mkubwa wa Ruvu Juu ambao umeongeza upatikanaji wa Maji kutoka Lita Milioni 82 na kufikia lita milioni 196. Mradi umekamilika Mwezi Aprili, 2017na unatoa huduma ya maji kwa Wananchi;

Kuendelea na uchimbaji wa visima 20 vya Kimbiji na Mpera ambavyo vitaongeza upatikanaji wa maji kwa lita milioni 260;

Kukamilika kwa miradi ya Visima 15 vya ufadhili wa Serikali ya Ubelgiji (BTC) ambayo inahudumia zaidi watu 250,000;

Kukamilika kwa miradi ya visima 10 vya mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Maji (BRN) ambayo inahudumia zaidi watu 120,000;

Kukamilika kwa miradi ya visima vya dharura vya DAWASA, Mapato ya ndani ya Manispaa, Mfuko wa Jimbo, Water Aid,TASAF,African Relief of Kuwait na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambayo inahudumia zaidi ya watu 230,000.

Matarajio ya Mkoa ni kuwapatia watu huduma ya Majisafi kwa asilimia 95 ya wakazi wote na uondoshaji wa Majitaka kwa asilimia 30 ifikapo mwezi Desemba 2025.

  • Changamoto Katika Utoaji wa Huduma ya Maji pamoja na Mkakati ya Kukabiliana na Changamoto hizo.

Changamoto kubwa katika utoaji wahuduma ya maji katika Jiji la Dar es Salaam ni kasi ndogo ya uwekezaji ukilinganishwa na kasi kubwa ya ongezeko la watu. Ongezeko kubwa la watu Jijini hasa kuanzia miaka ya 1980 kwa kiasi kikubwa limechangia katika kuongeza mahitaji ya maji. Changamoto zingine ni pamoja na:-

S/No
CHANGAMOTO
MIKAKATI
1
Upanuzi wa mtandao wa DAWASA kutokukidhi ya mahitaji wa wakazi wa Jiji
Mtandao wa kusambaza maji kutoka visima 20 vya Kimbiji na Mpera ujengwe
2
Upatikanaji wa maeneo ya
kujenga miundombinu
Kuendelea kuwasiliana na Wadau ili kupata maeneo ya kujenga miundombinu ya maji na pia kutumia way leave zilizopo kwa kukubaliana na Taasisi husika
4
Ukuaji na ujenzi holela wa
makazi,
Ushirikishwaji wa Jiji, Manispaa na Wizara ya Ardhi katika Upangaji wa Miji.
5
Wizi wa maji, uharibifu na wizi wa miundombinu ya Majisafi na Majitaka,
unachangia kiwango kikubwa cha maji yasiyolipiwa
Kushirikiana na wananchi, vyombo vya ulinzi na usalama katika kulinda miundombinu na kuzuia wizi wa maji na uharibifu wa miundombinu na uchafuzi wa maji.
6
Watumiaji maji kutokulipa
Ankara za maji kwa wakati,
Kuweka dira za maji kwa wateja wote, usomaji wa dira za maji kufanywa kwa kutumia vifaaa maalum vya kuchukua kumbukumbu (data loggers) ili kupata takwimu sahihi.
7
Gharama kubwa za uendeshaji ikilinganishwa
na makusanyo,
Gharama za maji ziende sambamba na Gharama za uzalishaji maji pamoja na uwekezaji;
8
Mfumo wa kuondoa majitaka haujafika maeneo mengi ya Jiji (unakidhi asilimia 10 tu)
  • Ujenzi wa miundombinu ya Majitaka kukidhi asilimia 30 ya mahitaji unahitajika
  • Mradi wa kujenga mifumo mikubwa 3 (Jangwani, Mbezi Beach na Kurasini ) na
  • Ujenzi wa mifumo midogo 50 ya kusafisha Majitaka chini ya Programu ya Maerndeleo ya Sekta ya Maji, mradi huu utaanza Julai 2017
9
Ufinyu wa bajeti/kuchelewa kutolewa fedha za kutekeleza miradi mipya ya maendeleo
Serikali inaendelea na utafutaji fedha kutoka kwa Wadau wa Maendeleo na kutenga kwenye bajeti kwa ajili ya Utekelezaji miradi mikubwa.
10
Migogoro ya uendeshaji Miradi ya Maji ya Jamii inayosimamiwa na Jumuia za Watumia Maji (COWSOs).
Tathmini imefanyika kuona namna bora ya usimamizi wa miradi ya Jamii. Miradi inayotumia mtandao wa DAWASA na isiyo na utendaji mzuri, uendeshaji wake kuanza kuhamishiwa DAWASCO. Hadi sasa miadi 20 ya Jamii shughuli zake za uendeshaji zimekabidhiwa DAWASCO
11
Uchimbaji holela wa visima usiozingatia taratibu
Kuanzisha utaratibu wa kusajili visima na kutoa vibali. Lengo likiwa ni kupunguza magonjwa yanayosababishwa na maji kutoka kwenye visima visivyo na ubora. Zoezi hili linasimamiwa na Ofisi za Bonde la Wami Ruvu.

4.0. Mwisho

Tunatoa wito kwa Wadau na watumiaji wa huduma ya maji Mkoa wa DSM kulipia Ankara za maji kwa wakati, kuepuka wizi wa maji na uharibifu wa miundombinu ya maji, kulinda miundombinu iliyopo nainayojengwa ili huduma ya maji iwe endelevu. Aidha, ulinzi shirikishi wa vyanzo vya maji ni budi upewe kipaumbele katika ngazi zote, pia wananchi kutoa taarifaya ya uvujaji wa maji ili kuweza kupunguza upotevu wa maji.

"MAJI NI UHAI NA USAFI WA MAZINGIRA NI UTU"

JEDWALI NA I

  1. MIRADI INAYOTEKELEZWA KATIKA MANISPAA
Na
Jina la Mradi
Mtaa unaohudumiwa
Wateja waliounganishiwa majumbani
Vituo vilivyojengwa
Mfadhili
Idadi ya Watu wanaohudumiwa
Hali halisi ya mradi


Manispaa ya Ilala


1
Jumuia ya Watumia maji Kipunguni
Kipunguni B na Mji Mpya

37

12

WSDP

7,422

100%

2
Kivule/Shule ya Msingi
Kivule na Viwege

23

15

WSDP

6,138

100%

3
Pugu Bangulo
Bangulo

56

6

OWN SOURCE

6000

100%

4
Jumuia ya Watumia maji GOPU
Gongolamboto,Ulongoni B, Pugu Bombani, Dunda B, Bane na Guluka kwa lala

611

52

WSDP,BTC

29,666

100%

5
Ulongoni A
Ulongoni A

53

4

Mfuko wa Jimbo

2,318

100%

6
Jumuia ya Watumia maji Kitunda Relini
Kitunda Relini

218

11

African Relief of Kuwait

6,808

100%

7
Jumuia ya Watumia maji Kitunda C
Kiyombo

113

5

DAWASA

3,520

100%

8
Kitonga
Kitonga

22

3

Own Source

1,632

100%

9
Mkera
Mkera

-

3

Own Source

1500

90%

10
Lubakaya
Lubakaya

-

4

Own Source

2,000

100%

11
Lukooni
Lukooni

3

3

Own Source

1,518

100%

12
Usambazaji wa maji Pugu Kichangani
Kichangani

16

Own Source

8000

98%

13
Usambazaji  maji Kinyamwezi
Kinyamwezi,
Mustafa na Viwege

-

6

Halmashauri ya Jiji

3,000

100%

14
Jumuia ya Watumia maji Rada
Rada

16

3

Maendeleo ya Kata

1,596

100%

15
Mradi wa maji Pugu Station
Pugu Station

25

6

JICA, Own Source

3,150

100%

16
Mradi wa maji Segerea
Segerea

-

4

Own Source

2,000

100%

17
Mradi wa maji Kivule
Kerezange na Kivule

167

9

JICA

5,502

100%

18
Jumuia ya Watumia maji Twiga
Tabata Kisiwani na Kimanga darajani

50

13

BTC

6,800

100%

19
 Jumuia ya Watumia maji Ugombolwa
Ugombolwa

104

5

BTC

3,020

100%

20
Kisukuru
Kisukuru

-

-

Own Source, DAWASCO

2,500

85%

21
Jumuia ya Watumia maji Mzinga A
Mzinga

620

11

DAWASA/
WUA MZINGA

9,220

100%

22
Jumuia ya Watumia maji Mzinga B
Mzinga

270

2

DAWASA/
WUA MZINGA B

2,620

100%

23
Mradi wa maji Madenge
Madenge

56

4

Own Source

2,336

100%

24
Mradi wa maji Belege
Maruzuku

34

3

Own Source

1,704

Low yield

25
Mradi wa maji Mfenesini
Mnyamani

52

10

Own Source

5,312

100%

26
Mradi wa maji Buguruni moto
Kisiwani

12

3

DAWASA

1,572

100%

27
Jumuia ya Watumia maji Sharif Shamba
Sharif Shamba

10

9

Own Source

4,560

100%

28
Jumuia ya Watumia maji Mondo
Mivinjeni

26

3

Own Source

1,656

100%

29
Kinyerezi


9

BTC,DAWASCO

4500

100%

30
Mradi wa maji Tabata
Mtambani

-

3

Own Source

1,500

90%

31
Mradi wa maji Kitunda
Kipera

-

7

Own Source

3,500

85%

32
Mradi wa maji Virobo
Virobo

-

1

Own Source

500

85%

33
Mradi wa maji Tungini
Tungini

-

3

Own Source

1,500

50%

34
Mradi wa maji Majohe
Majohe

-

18

Own Source

9,000

35%

36
Mongolandege


5

DAWASA

2400

100%

37
Kipunguni B


5

DAWASA

2400

100%

38
FFU Ukonga


4

DAWASA

5700

100%

39
Kipunguni kwa Mkwelemba


5

DAWASA

3100

100%

40
Kivule Nyang’andu


4

DAWASA

3100

100%

41
Tabata Kisiwani


13

BTC

6500

100%



Manispaa ya Kigamboni


1
Minondo- Somangila
Minondo

10

FOOD Aid Counterpart

200

75%

2
Mwasonga Kisarawe II
Mwasonga

15

FOOD Aid Counterpart

200

90%

3
Ferry
Ferry

483

12

DAWASA, Water Aid

22,035

100%

4
Kibugumo
Kibugumo

99

9

JICA

4500

100%

5
Mjimwema/ Salanga
Salanga

71

9

JICA

950

100%

6
Tungi
Tungi/ Muungano.

225

9

Water Aid

5500

100%

7
Toamoyo
Toamoyo

272

4

Water Aid

5132

100%

8
Kigamboni
Kigamboni

266

8

Water Aid

5416

100%

9
Chambewa
Chambewa

0

0

WSDP

938

35%

10
Malimbika
Malimbika/ Dege

0

0

WSDP

3047

20%

11
Kibene
Kibene/ Majengo

0

12

WSDP

5132

20%

12
Yale yale Puna
Punacenter/Moris/ Kibungo

28

25

JICA

2460

100%

13
Tundwisongani
Tundwi/ Songan/ Nyange

7

25

JICA

3721

100%



Manispaa ya Kinondoni


1
Makongo Mbuyuni
Makongo Mbuyuni

10

14

WSDP

3600

100%

2
Makongo Juu
Makongo Juu

0

2

World Bank/LGCDG

3500

100%

3
Tandale
Mtogole
Pakacha
Mkunduge
Mhulitani
Sokoni
Kwa Tumbo

80

21

BTC

5347

100%

4
Shule ya Msingi Changanyikeni
Changanyikeni

0

2

LGCDG

1900

100%

5
Mabwepande
Bunju B, Mji Mpya na Mabwepande

500

43

WSDP

11278

100%

6
Kigogo Buyuni
Kigogo Buyuni

0

1

Own Source

1617

100%

7
Kigogo Kati
Kigogo Kati

0

2

Own Source

2100

100%

8
Mivumoni
Mivumoni

0

1

Own Source

589

85%

9
Mtambani
Mtambani

18

1

Own Source

500

100%

10
Mwinyimkuu
Mwinyimkuu

26

3

Own Source

1250

100%

11
Magomeni Idrissa
Magomeni Idrissa

0

1

Own Source

305

100%



Manispaa ya Temeke


1
Toangoma
Goroka

154

14

WSDP

8,386

100%

2
Mbagala
Kizinga Bughidad

128

34

WSDP

17,152

100%

3
Chalambe
Mashine ya Maji

4

7

BRN

3,528

100%

4
Mianzini
Mianzini

133

27

WSDP

7,947

100%

5
Kibondemaji


3

Water Aid,PDF, DAWASCO

19500

100%

6
Mivinjeni


5

Own source

3000

100%

7
Makuka


18

Own source,TASAF

100%

8
Kiembe Samaki

33

8

TASAF

4,297

100%

9
Tandika/ Mabatini
Mabatini

8

WSDP

11000

95%

10
Sandali/ Mamboleo B
Mamboleo B na Kisiwani

8

WSDP

8000

95%

11
Azimio/Mbuyuni
Azimio

7

WSDP

11500

95%

12
Mamboleo A
Mamboleo A, Tindwa, Usalama

148

15

Water AID

8,332

100%

13
Dovya
Dovya, Msakala,Uwazi na Mbonde

402

12

BTC

11,379

100%

14
Mgembaki
Mbagala kuu, Kichemchem, Jeshi la wokovu, Mgeni nani

658

16

BTC

13,922

100%

15
Kiwika- Kijichi
Butiama, Misheni,na kijichi

464

31

BTC

17,426

100%

16

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa