• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

Wadau wa Maendeleo ni Muhimu katika Kuboresha Sekta ya Elimu

Posted on: August 14th, 2023

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe Angelah Kairuki amesema wadau wa maendeleo ni muhimu katika kuboresha sekta ya Elimu Nchini, ameyasema hayo leo Agosti 14, 2023 wakati wa kikao maalum na wadau mbalimbali wa elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam katika Ukumbi wa Anatoglo Mnazimmoja- Wilaya ya Ilala.

Akiongea wakati wa wa kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila amesema Mkoa umetekeleza maagizo ya Mhe Rais ya kukaa na wadau wa maendeleo hususani wadau wa elimu kwa lengo la kuhamasishana kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha miundombinu na mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji hapa nchini

RC Chalamila amesema Rais Mhe Dkt Samia ameendelea kufanya maboresho makubwa katika sekta ya Elimu kuanzia elimu Awali, Msingi, Sekondari hadi vyuo vikuu, ambapo elimu ya Awali hadi kidato cha sita elimu inatolewa bila malipo na vyuo vikuu wanafunzi hupatiwa mikopo ya elimu ya juu.

Hata hivyo idadi kubwa ya wanafunzi imekuwa ikiongezeka kutokana na maboresho yanayofanyika na Mhe Rais ambayo huamasisha wazazi wengi kupeleka watoto Shule na kuleta Changamoto ya kutokutosheleza kwa miundombinu ya shule ikiwemo vyumba vya madarasa, maabara, Maktaba, nyumba za walimu, vifaa vya kujifunzia na kufundishia, matundu ya vyoo na mabweni hivyo kikao hiki na wadau wa elimu kinalenga kutoa Suluhu ya Changamoto Katika Sekta ya elimu lazima tujiulize " Kama sio leo ni lini na kama Sio sisi ni nani" Alisema RC Chalamila

Kwa Upande wa Waziri wa OR-TAMISEMI amesema pamoja na mafanikio makubwa ambayo Serikali imeyapata katika sekta ya elimu bado kuna uhitaji mkubwa wa kuendelea kuboresha miundo mbinu ambapo takribani shilingi Trioni 17, 357,785,450,000.00 zinahitajika kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya elimu ya Awali, Msingi, Sekondari, shule za ufundi, elimu maalum, nyumba za walimu, na ukamilishaji wa miundombinu.

Hivyo Global Partnership for Education (GPE) wameendelea kusaidia Serikali ya Tanzania kupunguza Changamoto mbalimbali zilizoko katika sekta ya elimu nchini ambapo Tanzania imepata fursa ya kuomba ufadhili katika awamu ya tatu ambapo kigezo kikumbwa ni lazima wadau wazawa waonyeshe nia ya dhati ya kufadhili maboresho katika Sekta ya elimu kwa kujitoa kuchangia maboresho hayo.

Vilevile OR-TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya elimu inaendelea na maandalizi ya hafla ya kuhamasisha wadau wa ndani Kufadhili maboresho ya sekta ya Elimu hafla ambayo inatarajiwa kufanyika Mkoa wa Dar es Salaam tarehe 31/08/2023 Mgeni rasmi anarajiwa kuwa Mhe Jakaya Mrisho Kikwete Rais Mstaafu


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Temeke Yang'ara Mwenge wa Uhuru 2025

    June 02, 2025
  • RC Chalamila: Miradi 36 yenye Thamani ya Tsh 79,255,160,719.44 Kupitiwa na Mwenge wa Uhuru Dar

    June 01, 2025
  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa