• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

Ujenzi wa Dharura Barabara ya Kimara- Bonyokwa Uanze mara Moja

Posted on: November 13th, 2023

Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa Pamoja na Mkuu wa Mkoa Mhe Albert Chalamila leo Novemba 13, 2023 wamefika katika barabara ya Kikwete High way itokayo Kimara mwisho kuelekea Bonyokwa kuona changamoto zinazowakabili watumiaji hususani katika Kipindi hiki cha mvua ambacho kimechangia uharibifu mkubwa

Wananchi walijitokeza kwa wingi kuelezea kero na changamoto wanazopata zikiwemo kukosa huduma ya afya, nauli za bajaji na bodaboda kupanda, biashara zao kukwama na zaidi kila mwaka wanapewa majibu ya kiasa wanapohitaji utatuzi wa changamoto zao.

Mhe Innocent Bashungwa aliwahakikishia wananchi wa maeneo hayo kwamba mkandarasi anatakiwa kuanza ujenzi wa barabara hiyo yenye KM 7 kwa kiwango cha lami mwezi Desemba mwaka huu pia ametoa agizo ujenzi wa dharura uanze mara moja, "Ninakuelekeza meneja TANROAD gusa mfuko wako wa dharura tafuta mkandarasi ambaye wakati wananchi wamelala yeye anatengeneza hii barabara."

Mhe. Chalamila alitilia mkazo suala la ujenzi huo uanze muda huohuo kwa kuagiza meneja wa TANROADS abaki pale kuanza kazi na ifikapo kesho jioni atapita kukagua na kuwachukulia hatua iwapo hawatafuata maelekezo waliyopewa, "Kwakuwa Mhe Waziri amesema wakatafute hela ya dharura, nataka niwaahidi kesho jioni, saa mbili ya usiku nitakuwa hapa," alisema RC Chalamila.

Vilevile RC Chalamila amewataka watumie 'molam' ili kuepuka utelezi kwa watumiaji, ni muhimu kurudisha mawasiliano kati ya pande hizo mbili, matatizo wanayokumbana nayo ni makubwa  na Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan bado ana mipango mingi ya utoaji wa fedha ili kuendelea kutatua kero za muda mrefu na zile za muda mfupi kwa mwananchi.

Naye mbunge wa jimbo hilo la Ubungo Prof. Kitila Mkumbo alisema kwamba wananchi wanapokuwa na shida wana haki yakuwalaumu viongozi wao na kuwaomba wawe na subira kwakuwa barabara hiyo imeshaingia kwenye mpango na suala hilo lishafika bungeni na ipo kwenye bajeti.

Awali mhe. Bashungwa na RC Chalamila walifanya ziara kata ya Kibamba na kukagua ujenzi wa barabara inayoanzia Kibamba Shule kuelekea Mpiji Magohe yenye urefu wa KM 9.2 ambayo ishakamilika KM 2 huku KM 1.5 ujenzi wake unaendelea. Sambamba na hapo walifika mpaka Kiluvya kukagua mchakato wa ujuenzi wa barabara ya mwendo kasi inayotarajiwa kufika mpaka kibaha

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa