• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Atatua Kero za Wananchi wa Kawe

Posted on: August 30th, 2021

Baadhi ya wananchi wakisubiri kuwasilisha kero zao katika uwanja wa Tanganyika Perkers Jimbo la Kawe mapema leo.

- Wananchi wengi wajitokeza,kuelezea kero zao na kutatuliwa papo hapo

-Atembea na Wataalamu wa Idara zote kutoka Sekretarieti ya Mkoa, Manispaa ya Kinondoni, LATRA na POLISI

 Aahidi kwenda na Waziri wa Ardhi na Kamishna- Mabwepande

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla Leo tarehe 30 Agosti, 2021 ameanza ziara rasmi ya kupita Jimbo kwa Jimbo katika Mkoa huo ili kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua papo kwa papo.

Mhe. Makalla ameanza na Jimbo la Kawe lililopo katika Wilaya ya Kinondoni ili kuwafuata wananchi waliopo pembezoni ambapo ndipo kwenye changamoto nyingi.

Akiwa katika Jimbo hilo Mhe. Mkuu wa Mkoa alishuhudia umati Mkubwa wa wananchi uliofika mahali hapo ili kutatuliwa KERO zao.

Mhe. Mkuu wa Mkoa alipokea KERO mbalimbali zinazohusu Ubovu wa Barabara, Migogoro ya Ardhi, Mafuriko,Ukosefu wa maji katika baadhi ya kata,wananchi kubomolewa nyumba zao bila utaratibu, Ukosefu wa shule kwenye baadhi ya maeneo , dhuluma ya Fedha za watu katika ununuzi wa Viwanja, Kelele za Baa na ucheleweshwaji wa upatikanaji wa Ajira.

Mhe. Makalla kupitia Wataalamu wake wa Mkoa, Manispaa, LATRA, POLISI alihakikisha wananchi wote walioleta KERO zao wamepatiwa MAJIBU ya papo kwa papo na yale yaliyohitaji kufanyiwa kazi yapatiwe majibu ifikapo tarehe 6 Septemba, 2021.

Awali Mhe Amos Makalla alieleza kuwa Manispaa ya Kinondoni Migogoro Mikubwa sana ni ya Ardhi ambapo ameshuhudia eneo la Mabwepande ndipo penye Migogoro mingi hivyo kuahidi kwenda na Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi na Kamishna Ili kutatua KERO za huko.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amewaambia wananchi wa Kawe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan anatambua uwepo wa ziara hii na amesema KAZI IENDELEE aidha amepongeza uwepo wa miradi mbalimbali iinayoendelea katika Jimbo hilo na kusisitiza utolewaji wa taarifa kwa ngazi husika kabla ya utekelezaji wa Mradi.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa