• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makonda Aweka Mkakati wa Kuwaondoa Matapeli Wanaouza Nyumba na Mali za watu Kinyume na Taratibu

Posted on: September 25th, 2018

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo amekutana na Mabenki, Wenyeviti wa mitaa, madalali wa mahakama na mabenki kuweka mkakati madhubuti wa kudhibiti wizi na utapeli ambao umekuwa chanzo cha maumivu kwa wananchi.

Katika kikao hicho RC Makonda amewataka watu wa Benki kuhakikisha wanafanya uchunguzi na kujiridhisha kabla ya kutoa mkopo baada ya kuibuka kwa utapeli wa watu kutumia hati za watu na kuchukuwa mkopo pasipo muhusika kujua jambo linalopelekea nyumba na Mali za watu kupigwa mnada na kuacha familia zikikosa makazi.

Aidha RC Makonda amewataka madalali wa mahakama na wale wa mabenki kuhakikisha wanatoa taarifa kwa Wakuu wa Wilaya na Mwenyekiti wa mtaa kabla ya kufanya mnada huku akiwaagiza kuhakikisha wamesajiliwa na kuwa ndani ya chama cha madalali ili kuondokana na uvunjifu wa amani wakati wa minada.

Pamoja na hayo RC Makonda amewataka wenyeviti wa mitaa kusimamia sheria na taratibu kwa kuhakikisha minada inafanyika posipo uonevu wala uvunjifu wa amani.

RC Makonda pia amewaagiza watu wa Benki kuhakikisha Maafisa Mikopo na Wanasheria wao wanazingatia taratibu baada ya kubaini baadhi yao wamekuwa chanzo cha migogoro na utapeli.

Mbali na hayo RC Makonda amewapa mwezi mmoja watu wa Mabenki, Wenyeviti wa Mitaa, Madalali wa Mahakama na Mabenki kuandika changamoto na mapendekezo yao kisha kuyawasilisha kwake kwaajili ya kufanyiwa marekebisho na mwisho wa siku tuwe na sheria nzuri inayomlinda mkopeshaji na mkopwaji.

Hata hivyo RC Makonda amewataka wote wanaokopesha wananchi mitaani kienyeji pasipo kusajiliwa wala kuwa na vibali vya utambuzi kuacha Mara moja kwakuwa wamekuwa chanzo cha migogoro huku akiwataka madalali wa nyumba,viwanja na mashamba kuhakikisha wanasajiliwa na kutambulika na serikali.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa