• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC MAKONDA ATOA RUNINGA 69 KWA MAGEREZA NA HOSPITALI ZA DAR, AJUMUIKA NA WAFUNGWA KWENYE CHAKULA CHA PAMOJA

Posted on: December 9th, 2017

Mkoa wa Dar es Salaam ameadhimisha Siku ya Uhuru kwa Kuwatembelea Wafungwa na Maabusu kisha kupata Chakula cha Pamoja na kutoa huduma ya Masaada wa Kisheria na Ushauri Nasaha kwa Wafungwa na Mahabusu.

Katika Maadhimisho hayo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. PAUL MAKONDA ametoa Msaada wa Runinga za Kisasa 69 (Flat Screen) Touch zenye ukubwa wa Inch 40 kwa Magereza na Hospitali zote za Mkoa wa Dar es Salaam ili kuwawezesha Wafungwa na Wagonjwa kupata haki ya kikatiba ya kupata Habari.

Hii ni Historia kwa Dar es salaam kuwa Mkoa wa kipekee wenye Runinga Magerezani zinazowawezesha Wafungwa na Mahabusu kupata Habari na Hotuba za Rais ili kuwapunguzia Msongo wa Mawazo ili wasiwe na Mawazo ya kujiua ambapo zitagawanywa kwenye Magereza ya Segerea, Keko na Ukonga. 

RC MAKONDA aliongozana na Viongozi wa Dini waliowafariji Wafungwa na Kuwafanyia Sala na Dua huku Watu wa Ustawi wa Jamii wakitoa Msaada wa Ushauri Nasaha kwa Wafungwa.

RC MAKONDA ambae amepokelewa kwa Furaha kubwa na Wafungwa wa Gereza hilo amewasihi kutokata tamaa kwa kuwa bado wanayo nafasi ya kutimiza ndoto zao baada ya kumaliza kifungo ambapo amewahimiza kuwa Mabalozi Wazuri kwa Jamii.

Ili kupunguza msongamano wa Mahabusu Gerezani RC MAKONDA amesaidia zaidi ya Mahabusu na Wafungwa 200 wa Gereza la Segerea kupata  Msaada wa Sheria ambao walikuwa hawana uwezo kifedha.

Aidha RC MAKONDA ametoa Magodoro 100, Vifaa vya Usafi na Sabuni za Kuoga na Kufua kwa Wafungwa na Mahabusu.

Baadhi ya Mahabusu na Wafungwa wamemshukuru RC MAKONDA kwa kuwa kiongozi wa Kwanza na wa pekee aliewatembelea na kupata chakula cha pamoja, kuwapatia Runinga, kusikiliza changamoto zao na kuwapatia Wanasheria na watu wa Ustawi wa Jamii kitendo kilichowafariji.

Aidha Wameshukuru pia kitendo cha RC MAKONDA kusikiliza changamoto zao na kuzipatia majibu ambapo wamemuahidi kuwa wamebadilika na watakuwa mabalozi wazuri kuhimiza jamii kuzingatia Sheria.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa