• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Rais Samia Amepiga "Hat Trick" Bajeti 2022/23

Posted on: June 15th, 2022

RC Makalla wa tatu Kushoto wakati alipozuru katika Soko la Kisasa Kibada Wilaya ya Kigamboni- Dar es Salaam mapema leo.

RC Makalla akikagua maendeleo ya ujenzi wa Hospitali maalum kwa ajili ya kutoa huduma za Afya kwa wagonjwa wenye kifua kikuu Sugu Kigamboni-DSM


- Ampongeza kwa bajeti 2022/23 imeenda kugusa wananchi wengi katika huduma Za jamii ikwemo Afya, Maji Na Elimu kwa kufuta ada kidato Cha tano Na sita.

- Asema Bajeti 2022/23 ni hat trick ni zaidi ya kuupiga mwingi

- Fedha Za miradi ya maendeleo zinatolewa kwa wakati na hakuna mradi umesimama

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa Bajeti kuu ya Serikali kwa Mwaka 2022/23 ambapo amesema Bajeti hiyo imegusa Maisha ya Wananchi wengi katika Jamii hususani sekta za Elimu Baada ya kutangaza kufuta ada ya kidato Cha tano na sita.

RC Makalla amesema hayo alipotembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa Ujenzi wa Hospital ya Rufaa ya Kifua Kikuu Kanda ya mashariki inayojengwa Vijibweni Wilayani Kigamboni ambapo kukamilika kwake itasaidia Wananchi wa ukanda huo.

Aidha RC Makalla amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zaidi ya Shilingi Milioni 688 za Ujenzi huo ambao kwa Sasa umefika Asilimia 40 na unatajariwa kukamilika mwishoni mwa mwezi October mwaka huu.

Pamoja na hayo RC Makalla amesema Hospital hiyo itakuwa na uwezo wa kupokea na kuhudumia Wagonjwa 80 kwa siku na itakuwa na Madaktari bingwa wa kutosha.

Wakati huohuo RC Makalla ametembelea Ujenzi wa Soko la kisasa la Kibada lililogharimu Shilingi Bilioni 6.3 ambalo Ujenzi wake upo Asilimia 99 kukamilika ambapo litaanza kutumika muda wowote kuanzia sasa.

Ili kuhakikisha Biashara zinafanyika, RC Makalla ameelekeza Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni kuweka Mazingira Bora ya kuchochea biashara ikiwa ni pamoja na Miundombinu ya Barabara za kuingia na kutoka.

Hata hivyo RC Makalla amesema kuwa Soko Hilo Lina uwezo wa kupokea Wafanyabiashara 1,000 ambapo amepongeza *ubunifu wa Ujenzi wa Vizimba na kabati za kuhifadhi mizigo.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Temeke Yang'ara Mwenge wa Uhuru 2025

    June 02, 2025
  • RC Chalamila: Miradi 36 yenye Thamani ya Tsh 79,255,160,719.44 Kupitiwa na Mwenge wa Uhuru Dar

    June 01, 2025
  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa