• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Atangaza Kumaliza Mgogoro wa Ardhi Kata ya Mabwepande

Posted on: August 10th, 2022

 

- Aelekeza Ardhi iliyovamiwa zaidi ya Ekari 6000 za NSSF na DDC zirasimishwe kwa kupima viwanja na Wananchi kununua viwanja hivyo

-Aagiza kila Taasisi inayomiliki eneo Jumatatu Agosti 15,2022 wafike Mabwepande kuhakiki mipaka yao na kuyalinda maeneo hayo

-Asema Uamuzi umezingatia mapendekezo 19 ya kamati ya wataalam aliyoiunda kushughulikia mgogoro wa Ardhi zaidi ya Wananchi 4000 waliofika na kuhakikiwa na kamati

-Wananchi wa Mabwepande wamefurahishwa na kupongeza Uamuzi wa Serikali

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Amos Makalla leo Agosti 10,2022 *ametembelea na kukagua zaidi Ekari 6000 za NSSF na DDC ambazo zimevamiwa na Wananchi Kata ya Mabwepande Kinondoni-Dar es Salaam.

RC Makalla akiongea na umati wa Wananchi katika viwanja vya Kata ya Mabwepande baada ya kukagua eneo lililovamiwa *ametangaza rasmi kumaliza mgogoro wa Ardhi Kata ya Mabwepande kwa kutoa maelezo yafuatayo.

Mosi RC Makalla ameelekeza Ardhi iliyovamiwa na Wananchi zaidi ya Ekari 6000 za NSSF na DDC Kurasimishiwa na kupimwa viwanja na Wananchi wapewe fursa ya Kuzinunua viwanja hivyo kipaumbele kiwe kwa wananchi wa eneo hilo.

Aidha RC Makalla ameagiza kila Taasisi inayomiliki eneo Mabwepande Jumatatu Agosti 15,2022 wafike Kuhakiki mipaka yao na kuanzia hapo maeneo ya lindwe ili yasivamiwe tena.

Vilevile Mhe Makalla amesema Uamuzi alioufanya umezingatia mapendekezo 19 ya kamati ya wataalam aliyoiunda kushughulikia mgogoro wa Ardhi ambapo zaidi ya Wananchi 4000 walifikiwa na kamati na kuhakikiwa na uhakiki huo ulithitisha kuwa eneo hilo limevamiwa na kubaini wamiliki halali.

Hata hivyo kufuatia maamuzi hayo ya Serikali Wananchi wa Mabwepande wamefurahia na Kupongeza Uamuzi huo na kuahidi kushirikiana na Serikali bega kwa bega ili migogoro kama hiyo isitokee tena.

Ifahamike kuwa kumaliza kwa mgogoro wa Ardhi Mapwebande ni moja ya Migogoro mingi ya Ardhi katika Mkoa wa Dar es Salaam iliyomalizwa chini ya Uongozi imara wa RC Makalla toka ateuliwe na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Temeke Yang'ara Mwenge wa Uhuru 2025

    June 02, 2025
  • RC Chalamila: Miradi 36 yenye Thamani ya Tsh 79,255,160,719.44 Kupitiwa na Mwenge wa Uhuru Dar

    June 01, 2025
  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa