• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Akagua Mradi wa Zaidi ya Bilioni 52.1 Magomeni Kota

Posted on: September 8th, 2021

 

- Asema amejiridhisha majengo hayo bado hayajapangishwa.

- Aridhishwa na namna majengo yalivyojengwa yana kidhi mahitaji yote

- Afafanua kuwa kaya 644 ndizo zitapewa.

- Awaonya matapeli wanaowalaghai Wananchi kupangisha Kota hizo.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Amos Makalla leo Septemba 8,2021 amezuru na kukagua maradi wa ujenzi wa nyumba inayotekelezwa na TBA maarufu kwa Jina la *Magomeni Kota* Kinondoni Dar es Salaam.


Mradi huo kwa sasa uko katika hatua za mwisho kukamilika kinachomaliziwa ni mifumo ya Umeme katika eneo hilo kuna majengo ya gorofa 5 bustani na sehemu nzuri za michezo.

Mhe Makalla amesema amekuwa akipata taarifa nyingi wengine wanasema majengo tayari yameshapangishwa na wengine wakimuomba awasaidie kupata nyumba hizi, hivyo ujio wake ni kujiridhisha.

Mkuu wa Mkoa amejiridhisha kuwa hakuna aliyepangishwa, ameendelea kumpongeza Rais wa Tanzania  Mhe Samia Suluhu Hassan kwa dhamira yake ya kuendelea kutekeleza miradi iliyoachwa na mtangulizi wake, Magomeni  Kota ni moja kati ya miradi mingi inayotekelezwa hapa nchini.

Amebainisha kuwa wakazi waliokuepo katika eneo hilo wapatao kaya 644 ndio watakaopewa nyumba hizo na wataishi miaka 5 bila kulipa pango kama maelekezo ya awali yalivyokuwa.

Aidha ametoa onyo kwa matapeli kuacha kuwalaghai watu kuwa kuna nafasi ya kupanga katika majengo hayo.

Vilevile Mhe Amos Makala amewataka TBA kuwa na maono ya mbali au kuwa na mpango mkakati wa matumizi bora ya Ardhi katika eneo lililobaki kwani Dar es Salaam kwa sasa Ardhi haitoshi.

Ifahamike kuwa mradi wa Magomeni Kota ulianzishwa na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt John Pombe Magufuli na maagizo yake yalikuwa mradi ukikamilika kaya 644 ndio watapewa kipaumbele katika majengo hayo na wataishi kwa muda wa miaka 5 bure bila kulipa kodi.













ReplyForward






Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa