• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Aendelea Kutatua Migogoro ya Ardhi DSM

Posted on: December 17th, 2021

 - Amaliza Mgogoro wa Ardhi uliodumu kwa muda mrefu Boko Dovya kwa Somji- Kinondoni

- Atoa punguzo kwa Wakazi wa eneo hilo kuchangia Tsh 8,000/= kwa square mita moja badala ya Tsh 30,000/= bei ya Soko kwa sasa

- Wananchi wa mshukuru , Aelekeza Manispaa ya Kinondoni kuanza Mara moja mchakato wa upimaji na atakaye kamilisha apatiwe HATI yake

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Amos Makalla amemaliza Mgogoro wa Ardhi uliodumu kwa muda mrefu katika eneo la Boko Dovya kwa Somji -Kinondoni, Dar es Salaam

RC Makalla ametatua Mgogoro huo kwa njia shirikishi ambapo awali alizuru katika eneo hilo kujionea na kuwa na Mkutano na Wananchi kusikiliza mapendekezo yao, akiwapa fursa ya kuongea mmoja mmoja.

Baadaye akamkaribisha kamishna wa Ardhi Mhandisi Idrisa Kayera kutoa utaratibu wa Kitaalam wa gharama za upimaji wa Ardhi katika eneo hilo ambapo mtaalam anasema gharama ya mbweni Square mita moja kwa sasa ni Tsh 50,000/= hadi 80,000/= na Boko Bunju ni Tsh 25,000 hadi 35,000/= na gharama hizo zinatofautiana kutokana thamani ya eneo husika

Kwa Upande wa mtaalam wa Ardhi Manispaa ya Kinondoni wamesema wao wanatambua Gharama halisi za eneo hilo Kitaalam kama alivyosema Kamishna wa Ardhi lakini kwa kutambua gharama za Maisha kwa sasa wametoa pendekezo la mwananchi kuchangia Tsh10,000/= kwa Square mita moja ili aweze kupimiwa na kupatiwa Hati ya Ardhi

Aidha RC Makalla akatoa tamko la busara kwa kusema anawapunguzia Zaidi hadi Tsh 8,000 kwa Square mita ili wananchi hao waweze kuchangia na kuwataka wataalam kuanza mchakato huo mara moja na atakaye kamilisha apatiwe HATI yake.

Wananchi wamemshukuru RC Makalla na wamepongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Chini ya Rais Mhe Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali Wananchi

Ifahamike kuwa eneo la Dovya Kwa Somji lina ukubwa wa Square mita Milioni 1.4 ikiwa Serikali imetenga zaidi ya Square mita laki 2 kwa ajili ya huduma za Kijamii na Square mita zilizobaki ni kwa ajili ya makazi ya wananchi


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa