• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Makalla Achoshwa na Danadana za Mkandarasi Soko la Tandale

Posted on: January 19th, 2023

 

- Amtaka Mkandarasi kuongeza Kasi ya ujenzi.

- Mradi umeanza tangu mwaka 2019 lakini mpaka Sasa 2023 haujakamilika

- Mkandarasi anafanya mchezo wa kuleta mafundi siku akisikia Kuna ziara za Viongozi

- Serikali imemlipa Mkandarasi shilingi bilioni 7 kati ya 10 Lakini bado anasuasua.

- Wafanyabiashara walia Soko lao kuchelewa kuisha, Wanafanya biashara kwenye magumia

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla ameonyesha kukerwa na vitendo vya ubabaishaji wa Mkandarasi wa kampuni ya Namis Corporate Ltd anaejenga Soko la Tandale ambapo amemtaka kukamilisha ujenzi haraka.

RC Makalla ameshangazwa kuona mpaka sasa Mkandarasi amelipwa shilingi bilioni 7 kati ya bilioni 10 lakini bado ujenzi unasuasua ambapo Kwa mujibu wa mkataba Soko likitakiwa kukamilika mwaka 2020 Kisha kuongezewa muda mpaka January 2023 lakini bado ameshindwa kukamilisha na anaomba kuongezewa miezi 6 Tena jambo ambalo Mkuu wa Mkoa amekataa.

Kutokana na changamoto hiyo, RC Makalla ameelekeza Halmashauri ya Kinondoni kumsimamia kikamilifu Mkandarasi na kuwaonya wasimpatie kazi nyingine kwenye Halmashauri hiyo.

Aidha RC Makalla amemtaka Mkandarasi kuongeza idadi ya mafundi na kuhakikisha kazi zinafanyika Kila siku Ili Soko likamilike.

Kwa upande wako Wafanyabiashara wa Soko Hilo wamesema kwa muda mrefu wamekuwa wakifanya Biashara kwenye mazingira magumu kutokana na uweze mdogo wa Mkandarasi.

Ujenzi wa soko la Tandale ulianza Rasmi September 14 mwaka 2019 na likitakiwa kukamilika September 2020 Lakini ilishindikana kukabidhi Kisha Kuongezewa muda mpaka January 2023 ambapo Leo Mkuu wa Mkoa amefika na kukuta Soko halijakamilika

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Temeke Yang'ara Mwenge wa Uhuru 2025

    June 02, 2025
  • RC Chalamila: Miradi 36 yenye Thamani ya Tsh 79,255,160,719.44 Kupitiwa na Mwenge wa Uhuru Dar

    June 01, 2025
  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa