• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Chalmila Akutana na Viongozi wa Wafanyabiashara Kariakoo pamoja na Wadau wengine

Posted on: December 21st, 2024

 

-Wajadili hali ya usalama katika Soko la Kariakoo.

-Aeleza dhamira ya Mkoa kuwa na mpangilio mzuri wa wafanyabiashara katika eneo la Kariakoo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Disemba 21, 2024 amekutana na wadau mbalimbali wa Biashara katika eneo la Kariakoo pamoja na taasisi mbalimbali ikiwemo TANESCO, TANROAD, LATRA, DAWASA, Taasisi za fedha na Kamati ya Usalama ya Mkoa

Pamoja na mambo mengine kikao hicho kimejadili maswala mbalimbali yenye lengo la kuboresha ufanyaji biashara Kariakoo unaokidhi viwango vya kimataifa hususani hali ya usalama ambayo itawezesha biashara kufanyika saa 24, ambapo RC Chalamila ameipongeza Halmashauri ya Jiji kwa kuanza mchakato wa ununuzi wa Camera ambazo zinatarajiwa kufungwa maeneo mbalimbali ya mitaa ya Kariakoo.

Aidha Katika kupunguza msongamano kwenye eneo la kariakoo RC Chalamila amesema kupitia kikao hicho wamejadili mpango maalum shirikishi wa kuzuia aina zote za magari,bajaji na pikipiki kuingia katikati ya mitaa ya soko la kariakoo wakati wa asubui, mchana na jioni.

Vilevile RC  Chalamila amesema eneo la kariakoo ni muhimu kibiashara linahudumia Tanzania na nchi jirani hivyo magari yataruhusiwa kuingia nyakati za usiku pekee ili kupunguza msongamano na kuruhusu biashara kufanyika bila usumbufu asubuhi hadi jioni

Sambamba na hilo Mhe Mkuu wa Mkoa amesema ifike wakati Kariakoo iwe ni "Special Zone ya Kibiashara" mtu akitaka kufanya biashara lazima awe amekidhi vigezo vitakavyowekwa.      

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa Albert Chalamila amewataka wafanyabiashara na wadau wengine ikiwemo taasisi za fedha kuona namna ya kuongeza muda wa kufanya kazi hadi usiku hususani katika kipindi hiki cha kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka ili kutoa fursa kwa wananchi kupata huduma kwa urahisi zaidi

Sanjari na hilo amelitaka jeshi la polisi kuimarisha ulinzi kwa wafanyabiashara na wananchi katika kipindi hiki cha sikukuu ambapo amesema kwenye kipindi cha sikukuu za mwisho wa mwaka uhitaji wa bidhaa mbalimbali huongezeka kwa wananchi hivyo mpango huu wa kuongeza muda wa kufanya kazi utawezesha wananchi kupata huduma kwa urahisi

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa