• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Chalamila Msingi wa Malezi bora na Makuzi ya Mtoto ni Muhimu kwa Masilahi Mapana ya Taifa

Posted on: March 12th, 2025

 

-Amshukuru Rais Dkt Samia  kwa kuwa kinara katika kuhakikisha watoto wanapatata misingi bora ya makuzi, malezi na maendeleo yao.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila ameyasema hayo mapema leo Machi 12,2025 wakati akifungua kikao cha Tathimini ya utekelezaji  wa programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto-PJT MMMAM ( Naional Mult-sectoral Early  Childhood Development Program) kwa kipindi cha Oktoba- Desemba 2024.

RC Chalamila amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa juhudi kubwa katika kuhakikisha  kuwa watoto wanapata msingi bora wa  Makuzi, Malezi, na maendeleo yao.

Aidha RC Chalamila amesema kikao hiki cha tathimini ya utekelezaji wa PJT-MMMAM ni fursa adhimu ya kutafakari maendeleo yaliyopatikana katika kipindi  cha mienzi mitatu iliyopita, kujadili changamoto na kupanga mikakati ya kuboresha  utekelezaji wa Programu kwa kipindi kinachofuata

Kwa upande wa Katibu Tawala wa Mkoa Dkt Toba Nguvila akimkaribisha Mkuu wa Mkoa amesema Programu hiyo ilizinduliwa Dec 13, 2021 ikiwa na lengo la kuhakikisha watoto wanakua na kufikia kiwango cha juu kabisa cha  Maelezi, Makuzi  na Maendeleo yao ya awali ambapo amesema Mkoa unaendelea kufanya vizuri katika masuala ya lishe bora ambapo hadi sasa Mkoa uko katika kiwango cha chini kabisa cha udumavu hivyo kuna uwezekano mkubwa wa kuondoa kabisa changamoto hiyo.

Vilevile Dkt Toba Nguvila amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa wabunifu, na kutumia mbinu mbalimbali zenye kulenga kuifikia jamii kwa ukubwa wake.

Hata hivyo RC Chalamila amesistiza lazima tuhakikishe kila mtoto anapata hiduma bora za Malezi, Makuzi, na Maendeleo ya Awali ili aweze kufikia kilele cha maendeleo yake Kimwili, Kihisia, Kiroho na kijamii hii inawezekana kwa kuimarisha ushirikiano wetu, kuishirikisha jamii ipasavyo  na kuhakikisha rasilimali za kutekeleza programu hii zinapatikana.

Mwisho kikao hicho muhimu kimehudhuriwa na  Mganga Mkuu wa Mkoa, mratibu wa programu jumuishi, viongozi wa Dini, waratibu na wataalamu wa programu hii ngazi za Halmashauri, Watalaam kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na wadau wengine wa utekelezaji wa programu ya MMAM kutoka katika mashirika ya kimataifa, Kitaifa na Asasi za Kiraia

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa yakagua Miradi ya Maendeleo Wilaya ya Temeke

    May 07, 2025
  • RC Chalamila Aongoza Maadhimisho ya Mei-Mosi Dar es Salaam.

    May 01, 2025
  • Dkt Hussein Ally Mwinyi Aweka Jiwe la Msingi Barabara ya Kiibada, Mwasonga-Kimbiji

    April 25, 2025
  • RC Chalamila Dar ni Salama Aeleza Mafaniko na Mipango ya Maendeleo ya Mkoa

    April 18, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa