• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Chalamila Atoa Ufafanuzi wa Uhaba wa Sukari Nchini

Posted on: February 19th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Februari 19, 2024 akiwa katika Mkutano wa hadhara Wilaya Temeke Jimbo la Mbagala ametoa ufafanuzi kwa wananchi juu ya uhaba wa Sukari hapa nchini na jitahada za Serikali Chini ya kiongozi mahiri Dkt Samia Suluhu Hassan katika kukabiliana na Changamoto hiyo.

RC Chalamila amesema si kweli hata kidogo kuwa Serikali haina majibu kuhusu uhaba wa Sukari pia sio sahihi kuwa Sukari haipatikani kwa sababu kuna wafanyabishara wameficha, ukweli ni kwamba katika Kipindi cha mwezi wa kumi na moja, kumi na mbili mwaka jana na mwezi wa kwanza mwaka huu viwanda vya ndani havikufanya uzalishaji wa Sukari

Sababu kubwa ya viwanda kutofanya uzalishaji hususani kiwanda cha Kilombero, mtibwa, kiwanda cha Moshi, Bagamoyo na Dakawa ni kutokana na mvua kubwa zilizonyesha katika mashamba ya miwa maji yalijaa na barabara ziliharibika kwa kiasi kikubwa ambapo hakuna magari yaliyoweza kuingia kwenye mashamba hayo.

Hivyo kutokana na kadhia hiyo uzalisha wa Sukari ulikuwa hafifu kwa kuwa miwa ikiwa katika hali nzuri tani 10 huweza kuzalisha Sukari tani 1 na miwa iliyoko kwenye maji tani 18 huweza kuzalisha Sukari tani 1.

Aidha RC Chalamila amefafanua kuwa kiwango cha Sukari ambacho kingekuwa toshelezi na ndicho kilichopangwa kwa nchi ya Tanzania ni tani 555,000 wakati kiwango cha sukari mwaka huu kilichopatikana ni tani 520,000 tu

Kwa kutambua Changamoto hiyo Serikali Chini ya Rais Dkt Samia Suluhu iliamua kuagiza Sukari nje ya nchi, India na Brazil takribani tani 100,000 na Sukari hizo zinaingizwa hapa nchini pasipo kulipa kodi ya ushuru wa forodha pia bila kodi ya ongezeko la thamani hivi vyote vinafanywa na Serikali ikiwa ni jitihada za kukabiliana na uhaba wa Sukari hapa nchini.

Mwisho ni ukweli usio pingika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi mahiri wa Dkt Samia Suluhu Hassan ni Serikali sikivu " tusiwasikilize wapotoshwaji wasiolitakia mema Taifa letu" alisistiza RC Chalamila.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila: Miradi 36 yenye Thamani ya Tsh 79,255,160,719.44 Kupitiwa na Mwenge wa Uhuru Dar

    June 01, 2025
  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa