• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Chalamila Ataka Wananchi Kutumia Taka kama Fursa ya Kujipatia Kipato

Posted on: February 21st, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila ameyasema hayo leo Februari 21,2024 alipotembelea kiwanda cha chupa za plastic zilizotumika eneo la viwanda Mikocheni Wilaya ya Kinondoni.

RC Chalamila akiwa katika muendelezo wa ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kusikiliza kero za wananchi katika Wilaya zote za Mkoa huo ikiwa leo ni siku ya tatu toka aanze ziara yake.

Mhe Albert Chalamila ameridhishwa na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika jimbo la Kinondoni kama vile miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa, na kituo cha afya.

 Aidha RC Chalamila amesema ni wakati muafaka kila mwananchi akitazama taka imjie fedha, imjie Ajira, imjie Nishati pia imjie namna bora ya kuweka jiji safi

Kwa kuwa jiji la Dar es Salaam lina kua kwa kasi sana ambapo linakadiriwa ifikapo 2030 litakuwa miongoni mwa majiji makubwa kati ya majiji 7 ya Afrika, hivyo ni vema kujipanga katika usafi vilevile upangaji mzuri wa miji yetu kwa kuwa haiwezekani kuwa Mega City wakati ni chafu na halijapangika.

Vilevile RC Chalamila amemtaka mwekezaji wa kiwanda cha chupa za plastic zilizotumika kufungua njia mara moja ambayo inalalamikiwa imezibwa kutokana na kulundika malighafi zake za chupa.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Bi Hanifa amesema Manispaa hiyo imeshatenga maeneo makubwa ya kuweza kuwekeza viwanda vya namna hiyo eneo la Mabwepande hivyo kila mtu ruksa kuomba.

Mwisho RC Chalamila amesema viwanda vya aina hiyo ni muhimu Katika jiji kwa kuwa husaidia kuliweka jiji safi wakati wote na kujikinga na magonjwa ya milipuko, wakati ni sasa tubadili fikra vilevile RC Chalamila anatarajia kuendelea na ziara yake katika Wilaya hiyo kesho Februari 22,2024 Jimbo la Kawe

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa