• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Chalamila Ataka Ubunifu wa Wataalam katika Kukabiliana na Uharibifu wa Mazingira

Posted on: June 5th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila amesema Katika kukabiliana na changamoto ya uharibifu wa mazingira Serikali ya Mkoa huo imekusudia kutoa mitungi ya gesi kwa wanawake miatatu (300) kwenye kila wilaya mkoani humo ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi na kuepuka ukataji miti

RC Chalamila amezungumza hayo Juni 5,2024 Jijini Dar es salaam katika maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani yaliyofanyika kimkoa wilayani kigamboni katika viwanja vya Mji mwema.

Mhe Albert Chalamila amesema matumizi ya nishati safi ndio nyenzo muhimu ya kukabiliana na uharibifu wa mazingira hasa ukataji miti hivyo mpango huo wa kugawa mitungi ya gesi utatoa hamasa ya utumiaji nishati safi

Aidha RC Chalamila amewataka wasimamizi wa misitu kusimamia vyema sheria za misitu ili kuepuka ukataji miti badala ya kusumbuka na wauza mkaa kwani mkaa hupatikana baada ya miti kukatwa hivyo nguvu kubwa ielekezwe kwenye kuzuia ukataji miti

Aidha Mkuu wa Mkoa Mhe Albert Chalamila amesema Rais Dkt Samia ambaye ni kinara wa Nishati safi katika utunzaji mazingira ameonesha njia na nia njema ya kutunza mazingira hivyo ni muhimu kumuunga mkono kwa vitendo

Kwa upande wake Meneja wa baraza la Taifa la uhifadhi na usimamizi wa mazingira NEMC kanda ya Temeke Anord Mapinduzi amesema siku ya mazingira duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo juni tano kufuatia shughuli za maendeleo kuanza kuathiri mazingira ambapo ilionekana ni muhimu kuikumbusha jamii kutunza mazingira hivyo amesisitiza wadau wote kuendelea kuungana kutunza mazingira kwa vitendo

Naye Capteni Rosimery David Katani Mkurugenzi mwendeshaji wa kampuni ya usafi ya SUMA JKT mmoja wa wadau wakubwa wa mazingira aliepatiwa tuzo ya utunzaji wa mazingira ameahidi kuendelea kushirikiana na Serikali kwenye utunzaji wq mazingira kwa kuhakikisha anasimamia vyema usafi wa mazingira

Sanjari na hayo RC Chalamila amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa huo Dkt Toba Nguvila kukaa na wakurugenzi wa Halmashauri kuangalia namna bora ya kuboresha miundombinu ya Dampo la Pugu pamoja na kuja na mikakati ya kurejeresha taka kupitia wasomi walioko na wawekezaji.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa chama na Serikali, mamia ya wananchi, Kamati ya usalama ya Mkoa ikiongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa huo Dkt Toba Nguvila pamoja na mambo mengine maadhimisho hayo pia yalienda sambamba na utoaji wa tuzo kwa wana mazingira bora vilevile yamebeba kauli mbiu isemayo "Urejeshaji wa ardhi kupambana na hali ya jangwa na ustahamilivu wa ukame"

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila: Miradi 36 yenye Thamani ya Tsh 79,255,160,719.44 Kupitiwa na Mwenge wa Uhuru Dar

    June 01, 2025
  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa