• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

RC Chalamila Afungua Warsha Elekezi ya Maandalizi ya Dira ya Maendeleo ya Taifa

Posted on: July 20th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Julai 20, 2023 amefungua warsha elekezi ya maandalizi ya Dira ya maendeleo ya Taifa itakayotumiwa na Taifa letu kati ya mwaka 2025 hadi 2050.

Warsha hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Mikutano Anatouglo Mnazimmoja na kuhudhuriwa na Wataalam kutoka Wizara ya fedha, Sekretarieti ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakuu wa vyombo vya Usalama, Wakuu wa Taasisi za Umma, Taasisi binafsi, Taasisi za kiraia, Viongozi wa Dini na makundi maalum katika Mkoa huo.

RC Chalamila akifungua warsha hiyo amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa maandalizi ya machakato wa Dira mpya ya maendeleo ya Taifa kwani ni ukweli usiopingika Taifa lisilo na Dira ni Taifa mfu.

Aidha Mhe Chalamila amesema yako mambo muhimu ya kuzingatia ambayo Serikali imeanisha katika mchakato huo kama: Kuimarisha uchumi uliopo na kulinda mafanikio yaliyopatikana, matumizi ya fursa ambazo hazijatumiwa ipasvyo hadi sasa, Elimu ya Sayansi, Elimu ya ufundi na ufundi stadi, utafiti na Ubunifu ili kukuza ujuzi, kutavutia na kuasili teknolojia ili kukuza tija katika sekta zote za uzalishaji na kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi na kuingia ubia wa kimkakati.

Mdau kutoka taasisi binafsi akitoa maoni wakati wa warsha hiyo.

Vilevile kubaini uhalisia wa rasirimali zote, kujifunza kutoka nchi zilizoendelea kwa kasi kuanzia mwaka 1960 hususani bara la Asia na nchi nyingine zilizo jikwamua kutoka katika uchumi wa kati, pia wananchi wote watapata fursa ya kutoa maoni yao katika mchakato wa maandalizi ya Dira ya Taifa mpya inayotarajiwa kuleta maguzi makubwa ya kiuchumi na kijamii.

Hata hivyo Mhe RC Chalamila amesema makundi mahususi kama Bunge, mahakama, Sekta binafsi, Idara za Serikali, vyombo vya Usalama, Taasisi za Elimu, Asasi za kiraia, na Watanzania waishio ughaibuni, na washirika wetu wa maendeleo watapatiwa muda wa kutosha kushiriki mchakato huo muhimu pia wizara zote, Taasisi za Umma, wakala, idara zinazojitegemea, Sekretarieti ya Mkoa na Serikali za mitaa, sekta binafsi, wanadiaspora na wadau wa maendeleo wanatakiwa kutoa ushirikiano kwa timu ya maandalizi ya Dira mpya.

Sambamba na hilo Prof Samwel Wangwe amesema kufunguliwa kwa warsha hiyo kunaashiria kuanza uhamasishaji wa ushiriki wa wadau wote katika mchakato wa maandalizi ya Dira mpya ya Taifa ili waweze kutoa maoni ambayo yatafanikisha uandaji wa Dira hiyo kwa maendeleo endelevu


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa