• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

Rais Samia Anataka Anwani za Makazi Zitumike Kutoa Huduma Kidigitali - Mhandisi Mafuru

Posted on: March 20th, 2024

Na. James K. Mwanamyoto

Na. James K. Mwanamyoto
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Amani Mafuru amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amedhamiria anuani za makazi zirahisishe utoaji wa huduma kwa wananchi kwa njia ya kidijitali.
Amesema hayo jijini Dar es Salaam, wakati akifungua mafunzo ya utoaji wa barua za utambulisho kupitia mfumo wa kidijitali wenye kanzidata ya anuani za makazi (NaPA) yaliyotolewa kwa wenyeviti wa mitaa, watendaji wa mtaa, watendaji wa kata, waratibu wa anuani za makazi wa halmashauri na mratibu wa mkoa wa Dar es Salaam.
Mhandisi Mafuru amehimiza kuwa, Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais-TAMISEMI imetoa nafasi ya kipekee kwa halmashauri za mkoa wa Dar es Salaam kufanya zoezi la majaribio ya kutoa barua za utambulisho kidijitali na ndio maana inatoa mafunzo ya kuwajengea uwezo watendaji wanaotoa huduma hiyo.
“Azma ya Mheshimiwa Rais ni kuona Mfumo wa Anuani za Makazi unarahisha utoaji wa huduma ya barua ya utambulisho wa wananchi kidijitali,” Mhandisi Mafuru amesisitiza.
Naye, mshiriki wa mafunzo hayo Bi. Khadija Athumani ambaye ni Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Amana Kata ya Ilala amesema kuwa, anaishukuru Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia pamoja na Ofisi ya Rais-TAMISEMI kwa kuwapatia mafunzo yatayowarahishia utoaji wa barua ya utambulisho kidijitali hivyo kurahisisha utendaji kazi wao.
Kwa upande wake, Bi. Rozina Kimario ambaye ni Afisa Mtendaji wa Kata ya Manzese, Manispaa ya Ubungo amesema, wameyapokea mafunzo vizuri kwani barua za utambulisho watakazozitoa kidijitali zitawaondolea wananchi usumbufu kwani watapatiwa huduma hiyo popote walipo bila kulazimika kwenda kwenye ofisi ya mtendaji wa mtaa au kata.


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Temeke Yang'ara Mwenge wa Uhuru 2025

    June 02, 2025
  • RC Chalamila: Miradi 36 yenye Thamani ya Tsh 79,255,160,719.44 Kupitiwa na Mwenge wa Uhuru Dar

    June 01, 2025
  • RC Chalamila Ataka Machinga Kariakoo Kufungua Njia

    May 28, 2025
  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa