• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

Mapambano Dhidi ya Janga la Ukatili DSM ni Endelevu

Posted on: April 5th, 2024

 

-Asema vikao vya ulinzi wa mama na mtoto vitaketi mara nne kwa mwaka

-Abainisha watoto wa kiume wako kwenye hatari zaidi kufanyiwa ukatili

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Dkt Toba Nguvila ametaka kuendeleza mapambano dhidi ya ukatili wakinamama na watoto katika Mkoa huo kwa kuwa mkoa una idadi kubwa ya watu na muingiliano mkubwa wa watu hivyo ni vema kwa umoja wetu kushirikiana kutokomeza janga la ukatili hususani kwa kinamama na watoto " lakini sio kweli kwamba wanaume hawafanyiwi ukatili bali mwanaume akifanyiwa ukatili hatoi taarifa hivyo ni vizuri kwenda mbali zaidi ili kuwasaidia wanaume pia" Alisema Dkt Toba

Katibu Tawala wa Mkoa ameyasema hayo wakati akifungua kikao cha kisheria cha kamati ya ulinzi wa mwanamke na mtoto katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Aidha Dkt Toba amesema tunapaswa kufanya kazi kwa weledi, ubunifu katika kushughulikia maswala ya ukatili, ikiwa ni pamoja na kamati kufanya ziara katika wilaya za Mkoa kutoa elimu vilevile kufanya midahalo, vipindi vya elimu kwa umma katika TV na Redio.

Pia ni muhimu Kamati zihakikishe elimu ya ukatili katika jamii inafika hadi ngazi za chini kabisa katika mitaa, sambamba na hilo Katibu Tawala wa Mkoa Dkt Toba amesistiza ushirikiano katika kuratibu taarifa za ukatili hasa kwenye suala la Takwimu.

Kwa upande wa Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa bwana Nyamala Elisha amemuahakikishia Katibu Tawala wa Mkoa kusimamia kikamilifu maelekezo na maagizo yake ili kuleta ustawi katika jamii hususani wakazi wa Mkoa huo.

Mwisho baada ya kufunguliwa kikao hicho mada mbalimbali zimewasilishwa kwa lengo la kuijengea uwezo kamati hiyo ya ulinzi wa mwanamke na mtoto dhidi ya ukatili

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • RAS Nguvila Atoa Maagizo 14 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam

    May 16, 2025
  • Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa akiwasili NIDC-Kijitonyama

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa