• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

Kingatiba Dhidi ya Matende na Mabusha Kutolewa Dar, Octoba 24 - 29, 2021

Posted on: October 8th, 2021

 

- Kwa Mkoa wa Dar es Salaam Kingatiba itatolewa katika Halmashauri tatu (3)

- Rai yatolewa kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kupata Kingatiba ya Matende na Mabusha

- Kingatiba hiyo inatolewa kwa watu wote, watoto kuanzia miaka 5 na kuendelea

Katibu wa Afya Mkoa wa Dar es Salaam Sister Methew kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt Rashid Mfaume leo Octoba 8, 2021 amefungua warsha ya Wanahabari kuhusu ugawaji wa kingatiba za kudhibiti ugonjwa wa Matende na Mabusha kwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Kinondoni na Temeke

Warsha hiyo imefanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ilala boma, Dar es Salaam.

Akifungua warsha hiyo Katibu wa Afya Mkoa Sister Methew amesema Kingatiba dhidi ya Matende na Mabusha kwa Mkoa wa Dar es Salaam itafanyika katika Halmashauri 3, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Kinondoni na Temeke kuanzia Octoba 24 - 29 , 2021

Sister Methew amesema Kingatiba hiyo itafanyika katika maeneo mbalimbali yenye mikusanyiko ikiwemo mashuleni na kwenye vyuo.

Kwa kutambua umuhimu wa Wanahabari Sister Methew amesema ni daraja muhimu katika utoaji elimu kwa Umma na taarifa sahihi juu ya Kinga tiba dhidi ya Matende na Mabusha au Ngirimaji na ndio maana Wanahabari wamekuwa kundi mojawapo kupatiwa mafunzo ili wawe na uelewa na wakaelimishe Jamii.

Aidha Sister Methew ametoa Rai kwa Jamii hususani katika Halmashauri hizo 3 kujitokeza kupata kingatiba hiyo ambayo ni bure na tayari Mkoa umeshajipanga vizuri kutoka huduma kwa wananchi.

Kwa upande wa watoa mafunzo Bwana Oscar Kaitaba Afisa Mpango wa Taifa wa kudhibiti Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele, kwa niaba ya wataalam wengine amesema Jamii inapaswa kuelimishwa juu ya athari za Matende na Mabusha na Wanahabari ndio Wadau muhimu kupitia warsha hiyo wamepata uelewa juu ya Chanzo, Maambukizi, Ueneaji, na Kingatiba

Hivyo Jukumu la Wanahabari ni kwenda kuelimisha Jamii ili hatimaye kutokomeza kabisa Magonjwa hayo kwa kuwa watu watakuwa wameshajipatia Kingatiba hiyo.

Ifahamike kuwa kwa muda mrefu jamii imekuwa ikiteseka na magonjwa hayo pasipo kujua Kingatiba yake ipo na wengine wamekuwa wakiweka siri sasa ni wakati muafaka kwa Jamii kutumia fursa hii adhimu ya Kingatiba dhidi ya Matende na Mabusha au Ngirimaji


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa