• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Mkoa  wa Dar es Salaam

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Muundo wa Kiutawala
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Management,Monitoring and Inspection
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • TEHAMA
      • Government Communication Unit
  • Wilaya
    • Ilala
    • Kinondoni
    • Temeke
    • Ubungo
    • Kigamboni
  • Halmashauri
    • Jiji
    • Kinondoni MC
    • Temeke MC
    • Ubungo MC
    • Kigamboni MC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Muongozo wa Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu Mbalimbali
    • Taarifa Mbalimbali
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Bofya hapa
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio

Dar Mwenyeji Madhimisho ya Wiki ya Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa Yasiyoambukiza Kitaifa

Posted on: October 30th, 2023

 

RC Albert Chalamila wa katikati akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa Afya Mkoa na Wizara ya Afya ofisini kwake mara baada ya kuongea na waandishi wa Habari mapema leo

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Oktoba 30 ametoa taarifa kwa umma kupitia vyombo vya habari kuhusu maadhimisho ya wiki ya kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza Kitaifa Ofisi kwake Ilala Boma ambapo amesema Mkoa huo umepata bahati ya kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo.

RC Chalamila ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa huo na Mikoa Jirani kutumia fursa hii adhimu kujitokeza kwa wingi, kwa kuwa maadhimisho hayo mwaka huu 2023 yatatanguliwa na Kongamano la kisayanzi linalotarajiwa kufanyika katika ukumbi wa mikutano JNICC kuanzia tarehe 1-3 Novemba 2023, Mgeni Rasmi atakuwa Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa ambapo wataalam mbalimbali wa Afya kutoka katika Taasisi za Elimu na Utafiti watajadili mikakati mbalimbali ya kukabiliana na tatizo hilo " Wananchi na wadau mbalimbali mliopo katika Mkoa wa Dar es Salaam na nje ya Mkoa mjitokeze kushiriki Kongamano hili muhimu". Alisema RC Chalamila

Aidha RC Chalamila amesema baada ya Kongamano la kisayanzi Wananchi watapata fursa ya kupata huduma za upimaji Afya bure  pamoja na elimu ya kuzuia na  kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza, huduma hizo zitatolewa kwenye viwanja vya Mnazimmoja Wilaya ya Ilala kuanzia Novemba 11, hadi 18, 2023, " Wananchi jitokezeni kwa wingi katika maadhimisho hayo ikiwa ni pamoja na kujitokeza kupima afya zao Bure , Kinga ni Bora Kuliko Tiba" alisisitiza Mhe Chalamila

Tafiti nyingi zilizofanyika zinaonesha magonjwa yasiyoambukiza yanatokana na mabadiliko ya mtindo wa maisha katika Jamii, takwimu zinaonesha uwepo wa matumizi makubwa ya pombe ambapo asilimia 29.3 ya watu wana matumizi makubwa ya pombe, asimia 15.9 wanatumia tumbaku huku zaidi ya asilimia 97 hawazingatii ulaji unaofaa, vilevile RC Chalamila amemshukuru Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa katika sekta ya Afya ambao una masilahi mapana kwa Umma.

Dkt Rashid Mfaume akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa Habari kuhusu magonjwa yasiyoambukiza.

Kwa upande wa Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt Rashid Mfaume amesema maadhimisho ya mwaka huu yenye kauli mbiu " Usijisahau, Jali Afya Yako wataalam wa Mkoa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya wameshajipanga vizuri, ameendelea kutoa rai wananchi kujitokeza kwa wingi ambapo amesema taarifa za kitaalam zinaonesha vifo vinavyotokana na magonjwa yasiyoambukiza hapa nchini vimeongezeka ambapo kila vifo vitatu kimoja kinatokana na magonjwa haya aidha watu wanaopata magonjwa ya shinikizo la juu la damu imeongezeka mara 5 zaidi ndani ya Kipindi cha miaka 40 ambapo kwa sasa kila watu 4 mmoja anatatizo hilo.

Sambamba na hilo ikilinganisha na miaka ya 80 ilikuwa ni mtu mmoja tu mwenye tatizo hilo katika kila watu 20, hali kama hii inaonekana pia katika magonjwa mengine ya Saratani na kiharusi ambapo ongezeko ni kubwa kwa zaidi ya mara 9 ikilinganisha na miaka ya 80


Mratibu wa huduma za seli mundu kutoka Wizara ya Afya Bi. Asteria Mpoto wa kwanza kushoto akitoa ufafanuzi wa namna wizara ya afya ilivyojipanga kuealekea maadhimisho ya wiki ya magonjwa yasiyoambukiza ambayo kitaifa yanafanyika Mkoa wa Dar es Salaam.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU (MOCK) MKOA WA DARASA LA SABA - 2024 July 05, 2024
  • KARIBU MAKAMU WA RAIS WA MAREKANI MHE HARRIS KAMALA March 29, 2023
  • KARIBU MWENGE WA UHURU 2023 May 24, 2023
  • Matokeo ya Mtihani wa Mock Mkoa Darasa la Saba - 2020 September 02, 2020
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • CHALAMILA SERIKALI INATAMBUA NA KUTHAMINI KAZI YA UUGUZI

    May 23, 2025
  • Mchengerwa: Maafisa Habari Hakikisheni Wanachi Wanapata Habari Sahihi

    May 23, 2025
  • RC Chalamila Akabidhi Magari Mapya Mawili (2)-DSM

    May 20, 2025
  • Rais wa Finland Alexander Stubb Atembelea Machinga Complex - DSM

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

RC Chalamila Azindua Wiki ya Sheria DSM
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
  • Wilaya ya Ilala
  • Wilaya ya Kinondoni
  • Wilaya ya Temeke
  • Wilaya ya Ubungo
  • Wilaya ya Kigamboni

Tovuti Muhimu

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Ofis ya Rais-Utumishi
  • Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    Anuani ya Posta: S.L.P. 5429

    Simu ya mezani: +255 22 2203158

    Simu ya mkononi: +255 22 2203156

    Barua pepe: ras@dsm.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,haki zote zimehifadhiwa