Eneo linalofaa kwa kilimo na ufugaji ni hekta 107,500, ambapo Manispaa ya Temeke ni hekta 55,000, Kinondoni hekta 37,000 na Ilala hekta 15,000. Hadi sasa eneo linalotumika kwa kilimo ni Ha.32,972 sawa na asilimia 31 ya eneo lote.
Hali hii inatokana na maeneo ya mashamba kutwaliwa kwa ajili ya kupimwa viwanja vya makazi na wawekezaji.
|
Mazao makuu yanayolimwa ni mihogo, viazi vitamu, mpunga, mahindi, migomba na kunde. Mazao ya biashara ni korosho, minazi, mboga, matunda, maua na viungo. Mkoa utoa kipaumbele katika kilimo cha mboga matunda na viungo (high value crops) ambayo yana soko la uhakika hapa Jijini. |